Msanii wa Kikundi cha Sanaa cha Towero cha Manispaa ya Morogoro , Rajab Athuman ‘ Roja’ akionyesha umahiri wa kucheza na nyoka aina ya chatu , wakati wa onesho ya wasanii wa Kikundi hicho , siku ya Mahafali ya 17 ya wahitimu wa Ualimu wa Ufundi Stadi , ngazi ya Stashahada na Cheti katika Chuo cha Mafunzo ya Ualimu VETA Morogoro na kuhudhuriwa na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulungo, mjini Morogoro.

Msanii wa Kikundi cha Sanaa cha Towero cha Manispaa ya Morogoro , Rajab Athuman ‘ Roja’ ambaye ni bingwa wa akicheza na nyoka aina ya chatu , akiwaonesha baadhi ya wananchi sehemu aliyoumwa na Chatu huyo wakati wakimaliza onesho lao. Bahati chatu hana sumu kali, hivyo alinusurika. Na hii alisema si mara ya kwanza kung'atwa. Picha na mdau John Nditi wa Globu ya Jamii, Morogoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. hahahaaa wenzake huwa wanawatoa meno kabla ya kuwachezea!!!!

    ReplyDelete
  2. Mkome kuchezea majoka, usipoangalia mkono utakatwa huo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...