Watanzania Wenzangu,Mshiriki wetu katika shindano la Tusker Project Fame 2010 Peter Msechu amefanikiwa kuingia fainali za shindano hilo,kwa hiyo kikubwa kinachohitajika hapa ni kumpigia kura nyingi tu ili aibuke mshindi.Hivyo tumpigie kura mshiriki wetu PETER MSECHU kwa kutuma ujumbe mfupi,andika TUSKER9 halafu tuma namba 15522,kwa kufanya hivyo utakuwa umempa ushindi mshiriki wetu na pia kwa Tanzania.Kumbuka kura zinafungwa leo saa sita mchana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. will this work for any mobile phone? Will the Unyamwezini phones be able to transmit this vote? Is there an internet link?

    ReplyDelete
  2. kwa nini nimpigie kura? kwa nini nipoteze pesa zangu kwa kumnufaisha mtu ambae hata simjui na wala hanijui? kwa nini nipoteze pesa zangu kwa mtu ambao nina hakika akitoka hapo ni bichwa kubwa na kujiona wa maana?

    ReplyDelete
  3. Watanzania hatupendani, ndo maana kushinda kwa mtanzania ni ngumu maana hatupigi kura. Akishinda ni Tanzania imeshinda pia naye atakuwa ameinuka zaidi kimziki haijalishi unamjua au haumjui ni vizuri ukimuona mwenzako anapiga hatua ukamtia moyo na pia kumpongeza kuliko kumponda na kusema haumjui au atakusaidiaje. Tupendane wa tanzania

    ReplyDelete
  4. Mdau wa tatu tusidanganyane hapa, akishinda atakuwa ameshinda yeye na sio tanzania.

    ReplyDelete
  5. Akishinda itakuwa tanzania imeshinda? are you joking us? Kwanza sikumbuki watanzania kumchagua yeye au mwengine yeyote kutuwakilasha katika mashindano hayo, kwa maana hiyo officialy haiwakilishi tanzania.

    Pili hakuna suali la kutopendana au kupendana ni suali la kumpa kura unaedhani ni bora bila ya kuangalia passport zao, rangu yao au kabila lao. Kuna point gani ya kumpa ushindi kwa kuwa tu ni mtanzania ilhali unajua kuwa mganda ni hodari zaidi. Huko ni kumdanganya yeye na kujidanganya binafsi. Wacheni ubaguzi na muwe wa kweli mnapoamua kupiga kura. Asili ya mtu isihusishwe!

    ReplyDelete
  6. Mtoa Maoni:Sun Dec 05, 11:46:00 PM, Nakuunga mkono kabisa hapa sio ametokea wapi bali ni kweli uwezo wake ni mkubwa kuliko mganda, full stop sio ubaguzi hata kama hajui

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...