Mjumbe wa Bodi na mkuu wa Msafara wa timu ya Atreticco Paranaense toka chini Brazil,Rodevto Elias Karam (katikati) akiongea na vyombo vya habari leo asubuhi katika hoteli ya Movenpick kuhusiana na michezo yao miwili na timu za Simba na Yanga zitakazochezwa katika uwanja wa Taifa tarehe 18 - 20.Kushoto ni Mkurugenzi wa Timu ya African Lyon ambao ndio wenyeji wa timu hiyo hapa nchini,Nabil Salum na kuliani ni Kocha wa timu hiyo.
Mshauri Mkuu wa timu ya African Lyon,Ahmad Al- Shirazz akuzungumza wakati wa utambulisho wa ujuo wa timu ya Atreticco Paranaense ya nchini Brazil kwa waandishi wa habari waliofika leo katika ukumbi wa Kivukoni 1 ndani ya hoteli ya Movenpick jijini Dar leo.
Mjumbe wa Bodi na mkuu wa Msafara wa timu ya Atreticco Paranaense toka nchini Brazil,Rodevto Elias Karam akikabidhi jezi ya timu yake kwa Mkurugenzi wa timu ya African Lyon,Nabil Salum huku Mshauri Mkuu wa timu ya African Lyon,Ahmad Al-Shirazz akiangalia.
picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Simba na Yanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Br. Michuzi,

    Naomba niwapongeze African Lyon kwa juhudi zao za uhakika. Huu ni mwanzo mzuri na kusema kweli ndio changamoto kubwa wa vilabu vyengine kuiga mfano huu mzuri. Jambo la msingi linalojitokeza hapa ni Uongozi madhubuti pamoja na nguvu ya fedha na uwekezaji katika soka. African Lyon naamini sana kwamba itafika wakati nao watabadilishana jezi na timu ngeni kama hao wageni walivyowapa jezi yao. Aidha hili ni somo kwa vilabu vya Simba n Yanga kwamba watanzania wanataka bidhaa mpya mpya katika soka na si kupambwa katika magazeti na baadae uwanjani hauna burudani huku timu zikisheheni mapro. Kombe la Mapinduzi Zanzibar ni uthibitisho.TFF nayo ina haki ya kupunguza idadi ya wachezaji wa ligi wanaotoka nje ya Tanzania kwani ni vyema wawasaidie hawa viongozi ambao inaonekana dhahiri kwamba hawaelewi wanachofanya. Kujibebesha mizigo ya wachezaji wenye gharama kubwa wasio na tija kwa timu na kuwa chanzo cha mfarakano. Azam,African Lyon na wengineo wajitahidi katika kuleta ushindani wa soka la Tanzania.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...