
Wakati nipo darasa la tano, vijana ambao nilikuwa nawaona kwenye mitaa yetu, Gangstas With Matatizo (GWM), walikuwa wanatikisa na wimbo ‘Yamenikuta’ (ft. 2 Proud). Kwa hiyo, labda utaelewa kwanini naithamini sana Hip Hop.
Mwanzoni mwa miaka ya 2000… Juma Nature aliamua kuwashirikisha “GWM” na wasanii wengine, na kuunda kundi la Wachuja Nafaka. Bila shaka utakuwa unakumbuka ule wimbo ‘Mzee wa Busara’.
Baada ya albamu yao kutoka, mzee nikajipinda, nikabana hela ya matumizi shuleni na kununua kaseti ya Wachuja Nafaka. Ili tu niweze kusikiliza “malaria inapanda weeeeeeh, inapungua; inapanda weeeeeeh inapungua” muda wowote nitakaotaka!
Nadhani ile shilingi 700 niliyotumia kununua ile kaseti ilinipa zawadi ambayo sidhani kama kuna zawadi nyingine yoyote ile ambayo shilingi 700 nyingine itanipa. Kwenye wimbo ‘Ukweli na Uwazi’ kulikuwa na mistari ya msanii mpya kutoka Mwanza! Nikabaki kurudia kuusikiliza huo wimbo, hasa ubeti wa Fid Q.
kwa habari kamili nenda Vijana FM BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...