Home
Unlabelled
Vijana 711 WAHITIMU JKT 842 KJ MLALE, SONGEA LEO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
Hapa ndipo nilipofanya mafunzo yangu ya JKT, Ilikuwa ikiitwa operesheni miaka 30 ya uhuru. Mpo? wadau wa Lindipundipu, Lusonga, Magagula na Peramiho! namisi Ulanzi wa mitaa hiyo.
ReplyDeleteOMG! Old memories nimepiga kwata kwenye kambi hii Enzi za Kanali Mtono tulipiga sana Miraba ya Embakasi,mraba unauona unapoanzia unapoishia huuoni duh!enzi za maafande Kijanga,Agrey,na Nguvu ya Nyani hapo ni Kombania B,hapo C unamkuta Pilato. Si mchezo Lakini watu tulikuwa tunajongo vilevile.
ReplyDeleteSerikali idumishe JKT kwa kweli ni chombo kinachofunza sana maisha kwa Vijana.
Mdau London
Nawaungeni mkono wadau hapa juu. JKT ilikuwa ni shule ya aina yake. Nilikuwa Mafinga, Operesheni Jikomboe, mwanzoni mwa mwaka 1973.
ReplyDeleteIlikuwa kazi kweli, chini ya maafande kama Ngonyani, Chacha (walikuwa Chacha wawili), Ndabagoye, Mungure, Halima, na Izunya. Tulikula mchakamchaka, "fang fang" na kichura kama hatuna akila nzuri. Sitawasahau makuruta fulani ambao walikuwa hawakomi kuwakorofisha maafande na kuishia kwenye suluba nzito.
Ninashukuru kwa elimu niliyopata jeshini, ya masuala ya ukakamavu, masuala ya porini, silala mbali mbali na kufahamiana na watu kutoka sehemu mbali mbali za Tanzania. Nyerere alifanya kazi nzuri sana ya kujenga utaifa kwa njia hiyo.
Kwa mtazamo wangu, ingawa nimesoma shule na vyuo hadi kufikia kiwango cha juu kabisa, najivunia kwa namna ya pekee mafunzo ya JKT. Ningewakuta hao maafande wangu ningewaambia hivyo.
Shamba la Embakasi na mengine ya JKT yanatakiwa kuwa angalau ekari 20,000 ( elfu ishirini)kwa kutumia nyenzo za KILIMO KWANZA kama matrekta makubwa na JKT kuwa mfano wa kuwafundisha kilimo cha kisasa.
ReplyDeleteMambo ya ekari 200 karne hii ni kiduchu mno wenzetu utakuta mtu huko Guyana na ekari Milioni Moja kwa ajili ya ranchi ya mifugo ya kisasa ya familia yake.
Mdau
Aliyepitia JKT
kwanini wizaara ya habari na utamaduni? Wizara ya ulinzi wako wapi wao?
ReplyDeleteNIMEKUMBUKA ENZI ZANGU KWENNYE HII KAMBI,MDAU HAPA JUU UMENIKUMBUSHA ILE MIRABA YA EMBAKASI NA ZILE MBIO ZA MARATONI ASUBUHI KWENDA KUMWAGIA BUSTANI,ENZI YA MTONO, AKINA MAKARANGA PILATO,NA WENGINE.JKT JUUUUUUU.MDAU LONDON.
ReplyDeletenilikuwa nafikiria baada ya kufuta mambo ya form six kweanda JKT, Mlale ifungwa. Nakumbuka mambo ya lindipundipu, na afande Shaban compamia A, duu ilikuwa kali siyo mchezo. Mizigo ya kuni ilikuwa inaniua sana!!
ReplyDeleteAfante Shabani kombania A, na mambo ya lindipu mahindi ya kuchemsha kwenye debe, mizigo ya kini duu kweli JKT lazima iendelezwe nic chombo linachofunza maisha
ReplyDeleteSamahanini wana jamii, mimi ni kijana wa leo sasa haya mambo siyafahamu vizuri, ningepend kufahamu haya yafuatayo;-
ReplyDelete1.Haya mafunzo yanachukua muda gani?, mwezi 1,miezi 3,6,9,12 nk.
2.Mkiwa huko mnalipwa au mnalipa na kiasi gani? au ndio sifa za kijinga "Operesheni Uzalendo"
3. Nikitaka kujiunga natakiwa nifanye nini na niwe na sifa gani.
4.Baada ya kumaliza hatua hii watajiunga JW ngazi fulani au hapo ndio mwisho wa reli kisha wanaingia mtaani wakajijue huko?
5.Sehemu/kwenye mafunzo kama haya wafunzwa wa jinsia ya kike hua wanawakati mgumu aidha wajirahisishe kwa ngono au walazimishwe na wakufunzi kufanya hivyo, je huko hali ikoje kwenye hili swala.
6. Labda kama nimeona vibaya, hiikambi ilikua ya wanaume tuu, au hazitakiwi kuchanganywa jinsi zote mbili?
7.Naona wahitimu woooooote na huyu aliyeshika jambia wamekuja mikono ya sare/uniform zao, kwani hakuna sare za mikono mifupi kama ya huyo mkuu wa kikosi, au hio ndio sheria?
Ni hayo tuu ningependa kufahamu, ni mimi kijana wa leo ambaye ningependa kwanda kuchangamsha mwili na akili huko. Aksante