Mtaalamu wa Mambo ya kale katika chuo kikuu cha Colorado Denver,Dr.Charles Musiba akitoa maelezo juu ya nyayo za binadamu wa kale aliyeishi zaidi ya miaka Milioni mia tatu,zilizopo huko Laetoli,kijiji cha Enduleni,wilaya ya Ngorongoro leo.

Mtaalamu wa Mambo ya kale katika chuo kikuu cha Colorado Denver,Dr.Charles Musiba akimpa maelezo Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuhusu nyayo za binadamu wa kale aliyeishi zaidi ya miaka Milioni mia tatu,zilizopo huko Laetoli,kijiji cha Enduleni,wilaya ya Ngorongoro.Nyayo hizo zilifukuliwa hivi karibuni kwa maelekezo ya Rais aliyeshauri wataalamu hao kuzifukua na kuzihifadhi ili watafiti na watalii wa ndani na nje ya nchi waweze kuziona na kuendelea na utafiti wa kisayansi.Nyayo hizo ziligunduliwa na mtafiti wa mambo ya Kale Dr.Mary Leakey huko Laetoli mwaka 1978 na kufukiwa ili zisiharibiwe na mmomonyoko wa ardhi.(


JK akiangalia nyayo hizo. Picha zote na Woinde Shizza wa Globu ya Jamii



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Salaam,

    JAmani naomba nielimishwe! tunajuaje kama hizi nyayo au fuvu lina miaka million? mti una mizunguko unaweza kujua kwa kuona mizunguko je nyayo?

    ReplyDelete
  2. Hawa jamaa wa mambo ya kale mimi siwaamini sana, wanatumia kipimo kinaitwa carbon 14 kukadiria umri wa vitu vya kale. Hivi kweli nyayo zilizokanywagwa miaka milioni 3.6 zije zionekane mwaka 1978? I dought it.

    NB: Michuzi blog rekebisha maelezo, nyayo hizo ni za miaka milioni 3.6 iliyopita na si miaka milioni MIA TATU iliyopita.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...