Kampuni ya bahati nasibu ya Premier Betting kupitia mchezo wake wa Premier Bingo imekabidhi msaada kwa waathirika wa mabomu ya Gongo la Mboto msaada huo ni wa thamani ya shilingi milioni moja.
Akikabidhi msaada huo kwa mratibu wa misaada wa kituo cha Clouds FM Muhidin Mrope Meneja Masoko wa kampuni hiyo Afsa Hamad alisema kuwa kampuni ya Premier Betting imeguswa na matatizo yanayowagusa waathirika wa Gongo la Mboto.
Msaada huo ni mipira 22, kilo mia mia za mchele, sukari, maharage na gunia mbili za sabuni ya unga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...