Huku wakiwa na vikombe mkononi, baadhi ya wakaazi wa jiji la mbeya na vitongoji vyake na kutoka mikoa ya jirani Sumbawanga Iringa Songea wakiandamana kuuelekea ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mbeya kupinga kusitishwa kwa huduma ya matibabu ya magonjwa mbalimbali anayotoa kijana Jafari Willina leo
Wananchi wakiwa ofisi ya mkuu wa mkoa mbeya wakiwasubiri wawakilishi wao kuwapatia majibu toka kwa mkuu wa mkoa
Barua ya kusitisha huduma ya tiba ya asili kwa kijana Jafari Willina Iliyoandikwa na mganga mkuu wa halmashauri ya jiji la mbeya Dk Samweli Lazaro. Hadi tunaenda hewani jibu toka kwa mkuu wa mkoa lilikuwa bado hatujapata.

Picha zaidi na libeneke dada la Globu ya Jamii
BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. kwani nani alimpa Babu wa loliondo kibali cha kutoa tiba za asili?

    ReplyDelete
  2. Teh Teh!

    Ungesema imetoka kwa Mungu Dogo, wewe unasema imetoka kwa mama? Ona sasa, wakati wewe unaambiwa upeleke dawa yako Muhimbili, Serikali imepeleka wataalamu Loliondo 'kuomba' Dawa ili waipeleke Muhimbili.

    Pole Dogo, ulaji huooo.. unayoyoma!

    ReplyDelete
  3. Mnamuonea mbona Loliondo yeye hapelekewi barua? Ni kiwango gani yeye alipasi na huyu nin nini alichofail?

    kama ni kusimamisha simamisheni wote hata waganga wa kienyeji sio huyu tu...

    ReplyDelete
  4. Watanzania tumekuwa kama vivuli sasa tunafuata tuuuu. Serikali imeona ikomeshe maana ni muda mchache tu mngesikia maelfu ya watu wamepanga mstari mbeya kijijini huko aliko huyo dogo. Hivi hatuwezi ku reason out kwamba huu ni utapeli sisi wenyewe?

    ReplyDelete
  5. Loliondo tuliambiwa ni tiba ya kiimani, iweje hii ya Mbeya inakataliwa wakati ni ya kiimani?
    Au serikali sasa inaingilia imani za watu?
    Mnatonea sana sisi wananchi wa huku kusini kwa kuwapendelea wa kaskazini. Serikali onevu kabisa, sisi hatuna pesa za kutufikisha huko Loliondo za kukodi magari yenu ya watalii na kwenda kutalii kwa babu.

    ReplyDelete
  6. mmh wabongo bwana!Huyo dogo alikuwa wapi tangu zamani?Kwa hiyo anataka kutuambia mama yake alikuwa mganga wa kienyeji? au......tutanyweshwa mpaka sumu mwaka huu...mi nasema hivi walikuwa wapiii?

    ReplyDelete
  7. mwaka huu kazi ipo. Tutakunywa hata mavi ya tembo? DOGO!

    ReplyDelete
  8. Kwa kweli tuendako siko. Haya nami ngoja nibuni namna ya kuwavuna watu kwa staili ya dawa. Kumbe ni dili kubwa sana hilo!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...