Kaunta kuu ya Nyumbani Lounge, kiota kipya cha minuso na maraha kinachoendeshwa na Gadna G. Habash na Mai waifu wake Lady Jay Dee kilichopo Namanga, nyuma ya Best Bite Restaurant, mita kama 100 hivi kutoka barabara kuu, ama jengo la pili kushoto baada ya Virago.
Bufee la nguvu kila siku. Kwa mujibu wa Gadna G. Habash, kuanzia Jumapili hii kutakuwa na Menyu spesho ya Dozi ya Babu wa Loliondo (supu ya pweza) kwa mara ya kwanza maeneo hayo
Sehemu ya Nyumbani kama nyumbani vile...
Mambo mswano nyumbani
Karibu nyumbani

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Good job, hizi sehemu namna hii zinakosekana sana mjini hapa, lkn sijui utawezaje ku maintain decency, maana ukijaza watoto wakihuni wanaokunywa soda moja saa 6 mchana hadi saa 6 usiku sijui itakuwaje. ALL THE BEST GUYS!!!

    ReplyDelete
  2. hongera sana wapendanao nyie juhudi zenu zinapaswa kuigwa

    ReplyDelete
  3. Kweli Jide mjasiriamali, anataka mafuriko ya watu kwa kutangaza dawa ya babu..teh teh..kweli bongo lazima ubongoke la sivyo utaishi na umasikini milele. chemsha mwarobaini sema hii dawa ya babu watu watakunywa..500 kila kikombe au?

    ReplyDelete
  4. lol - dozi ya Babu wa Loliondo siyo? Very funny. Tutakuja!

    ReplyDelete
  5. Michuzi,bufee ni kiasi gani kwa kichwa?

    ReplyDelete
  6. Great job. Ila baadae badilisheni hivyo vitini havijatulia kihivyo.

    ReplyDelete
  7. ...Ankal Dawa ya babu inauzwaje hapo 'Nyumbani'?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...