Kaka Michuzi pole kwa kazi ya kuendeleza blogu ya jamii.

Mimi ninashida na anuani ya ubalozi wa Tanzania, Bangkok, Thailand. Nilijaribu kutafuta katika mtandao (Google) na nikapata anuani hii (Tanzania Honorary Consulate , Thailand, S.L.D. Condominium, 3rdFL., 501 Saladaeng 1, Rama IV Road,Bangkok10500,Thailand,
Phone: +66-2-2358282 ,+66-2-2358283 ,
Fax:+66-2-2361977).

Nilipofuatilia ubalozi katika anuani hiyo hapo nilipewa maelezo kwamba walishahama miaka 10 iliyopita! Sikukata tamaa na niliamua kuwapigia simu. Simu ikapokelewa na nikajibiwa kwamba hiyo line kwasasa inatumiwa na ubalozi wa New Zealand.

Kaka Michuzi, nimeamua nije hapa kwenye kwenye blogu ya jamii kwani inatembelewa na watu mbalimbali labda kuna mmoja wa wapenzi wa blogu hii anawezakua anafahamu anuani ya ubalozi wa heshima wa Tanzania kule Bangkok, Thailand.

Ombi langu ni kwamba, wadau wa libeneke (blogu ya jamii) tafadhari kama kuna mtu anafahamu anuani au hata namba ya simu nitapenda kufahamishwa! Natanguliza shukrani zangu za dhati.

Kwa yeyote mwenye anuani hiyo au namba ya simu ya mtu anaeshughurikia masuala ya kibalozi, Bangkok, tafadhari usisite kunifahamisha kwa kutumia barua pepe
52910601@st.kmutt.ac.th

Asanteni sana wadau wa blogu ya jamii.

Mdau wa blogu ya jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 01, 2011

    Nijuavyo mimi balozi wa Tanzania Thailand ni Mr Cisco ambae pia ndio balozi nchini Malaysia, wewe tafuta ubalozi wa Tanzania nchini Malaysia watakusaidia!

    ReplyDelete
  2. Mimi nipo Malaysia mwaka umepita sasa najua Malaysia kuna ubalozi wa Tanzania BUT nilijaribu sana ku google wala sijaupata matokeo yake napata this address
    Tanzania High Comission , Malaysia
    10/1 Sarv Priya Vihar
    110016
    New Delhi
    India
    Phone:
    +91-11-6853046
    +91-11-6853047
    Fax:
    +91-11-6968408
    Email:
    tanzrep@del2.vsnl.net.in
    Hata cjui kwa nini balozi zetu haziwezi kuweka mambo yake ktk order, hii ki2 always inanikera sana

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 01, 2011

    dah afafdhali ndugu yetu kwa kutusaidia kutuulizia!! sio wewe tu huko Thailand ila ni kila nchi ambayo huyu jamaa anasimamia sijui kfanya mipango gani atleast kuwatembelea raia waake!! labda tuwaulize wenzetu wa Malaysia kama kuna msaada wanaopata kutoka kwa ubalozi huu!! ninavyojua mh, cisco anatakiwa ahudumie malaysia, Philippines, Thailand, Laos na nyinginezo ila sijui kama kuna waliomwona au kusikia habari zake tangu alipoanza hiyo kazi. tunawaona wenzetu nchi nyingine wanavyoenjoy na maalozi wao hadi inaleta raha. Kule Philippines balozi wa Kenya huwa anawatembelea regulary ingawa nae ana ofisi yake Malaysia. kwa nini wakwetu hajulikani!!
    kama kuna wahusika wanasikia basi wajitahidi atleast kufanya jambo.
    Pole mdau wa Thailand suala ni kwamba usijisumbue kutafuta hapo hakuna lolote bali fuata ushauri wa mdau wa hapo juu kufuatilia malaysia maana utapoteeza muda wako. hakuna kitu kama hicho hapo hizi consul zilikufa kitaambo waliobaki hapo ni matapeli watakutoa hela zako wakijidai ni maajenti.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 01, 2011

    unajua sisi watu nchi yetu they dont care katika maswala kama haya. sasa adress imechange for almost 10 years, wameshindwa hata kuapdate new adress.... unajua inakera sana. kwa sasahivi hutoona umuhimi wake lkn ngoja upate shida ndo utajua. jirekebisheni serikali

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 01, 2011

    ndugu yangu labda balozi za huko asiya ndio zipo hivyo nyingi zipo tambarale tu nakushauri ndugu yangu nenda wizara ya mambo ya nje information office utapewa kilakitu ikiwezekana utampata hata desk oficer anaeshuhulikia maswala ya huko unako taka utapata maelezo yote

    ReplyDelete
  6. Proudly TanzanianMay 01, 2011

    Kwa huko Asia,far east tuna Balozi China na Malaysia. Hatuna Ubalozi Thailand. So, tafuta contact za Balozi hizo au wasiliana na Wizara ya Mambo ya Nje nyumbani...piga namba +255 22 2119054 begin_of_the_skype_highlighting              +255 22 2119054      end_of_the_skype_highlighting.

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 01, 2011

    BEIJING
    Embassy of the United Republic of Tanzania
    No.53 Dong Liu
    San Li Tun
    Beijing
    China
    Tel.: (86-10) 65322344, (86-10) 65321719, (86-10)65325572, Fax (86-10)
    5321695, (86-10) 65322394
    E-mail: tzbeijing@iuol.cn.net or tzbeijing@info.ioul.cn.net
    Accreditation to : People’s Republic of China, Thailand, Democratic People's Republic of Korea, Cambodia,Vietnam, Laos and Mongolia
    Source:http://www.tanzania.go.tz/embassies.htm

    ReplyDelete
  8. Proudly Tanzania; nilishatafuta sana hizo balozi za Tanzania nchini Malaysia but cjafanikiwa kuzipata umepita mwaka sasa naomba kama una address, or any contact zitakazonisaidia kuwapata

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 02, 2011

    Hizo emails hapo juu zoooooote, zinarudisha majibu zimefeli kuwa delivered! Simu hazipatikani!! Jamani jamani uwiiiii....Hivi wizara husika mnaliona hili?

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 03, 2011

    Mimi ni mtanzania ninaeishi THAILAND> NINAJITOLEA KUFANYA KAZI ZA KIBALOZI KWA HESHIMA YA TANZANIA. NAPENDA NIWASAIDIE WATANZANIA WAISHIO THAILAND NA NCHI ZA KARIBU. Ninaiomba wizara husika iwasiliane na mimi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...