Nahodha wa Simba Mussa Hassan Mgosi (shoto) akisalimiana na kubadilishana bendera na nahodha wa TP Mazembe kabla ya gemu huku waamuzi toka Sychelles wakiangalia
Simba na TP Mazembe kabla ya gemu

Simba SC leo imefunwga bao 3-2 na Tout Puissant Mazembe (zamani TP Englebert) katika mchezo wa mzunguko wa pili wa michuano hiyo Klabu Bingwa Afrika uwanja wa Taifa jijini Dar.

Katika mchezo uliopigwa wiki mbili zilizopita mjini Lubumbashi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), katika Uwanja wa Kenya, Simba ililala kwa bao 3-1, hivyo ndio kusema imefungwa jumla ya mabao 6-3.

Simba leo imejitahidi katika kukipiga na TP Mazembe ambapo mabingwa hao wa Afrika wana historia kwa kuwa timu ya kwanza kufika hatua ya fainali Klabu Bingwa ya Dunia, baada ya kuitoa Elan De Mitsoudje ya Comoro kwa mabao 4-2.

Simba ambayo ndio mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, huku wakiongoza ligi hiyo kwa pointi 44 sasa, walichesza kufa na kupona lakini vibopa hao wa Lubumbashi waliwazidi kete katika kila idara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. safi tu! midomo ilizidi...

    ReplyDelete
  2. Hakuna cha kusema Simba yaikosakosa TP Mazembe, Semeni tu imefungwaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!

    ReplyDelete
  3. Wamejitahidikwa kufungwa 3-2 Nyumbani,You are right Ankal!

    ReplyDelete
  4. Shehe naona utani unapitiliza. Mechi imetuuma, acha mzaha.

    ReplyDelete
  5. MATOKEO YALIJILIKANA MBONA TANGU MWANZO NANI ANAFUNGWA . IYO KUIKOSA KOSA NDIO KAULI ZETU ZA KAWAIDA WATAINZANIA . TUMEZOEA KILA SIKU , SJUI KUIKOSAKOSA , KUFA KISHUJAA NI VITU VYA KAWAIDA KIUKWELI HATUNA KIWANGO.

    ReplyDelete
  6. Simba mandemba...

    ReplyDelete
  7. Hivi jamani simba mnashindwa hata kuwa na kikosi cha tarumbeta kwa ajili ya kushangilia, mliona sie watoto wa mamba tulivyokuwa tumeuteka uwanja!???????????????

    ReplyDelete
  8. Tena bahati yetu timu ilibebwa na Waganda na wakenya waliomo kwenye timu. Huwezi kuwa na wachezaji wazuri wakati umefungia michezo mashuleni.
    Labda tukiandaa vizuri vijana baada ya miaka 8 ndiyo tunaweza kuwa na wachezaji wa-kitanzania wenye viwango.

    ReplyDelete
  9. Wamejitahidi kwa timu mabingwa kama wale kupigwa 6-3,wajipange upya

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...