Ankal akiwa na Deo Balile, Mhariri Mtendaji wawa Mtanzania wakiomba ufafanuzi kuhusu bei waliyonunulia, lini wataiwasha na je bei ya umeme watayowauzia TANESKO itakuwa sawa na ya Dowans wenyewe? Akaambiwa kwamba mkataba wao Symbion ni siri na muuzaji hivyo bei waliyonunulia hawawezi kuitaja. Kuhusu bei ya umeme itayouziwa TANESKO wamesema itakuwa poa na kwamba wataitangaza Jumatatu wanapotarajiwa kuwa na mkutano wa pamoja na kampuni hiyo. Kwa sasa wamesema wako tayari kuwasha umeme ila wanangoja treni la gesi la Songosongo lililoharibika lianze kazi na wao hawana noma wala nini na mambo ya siasa kwao hayana nafasi bali ni kazi tu na blah blah pembeni.  
Baada ya taarifa kwenye vyombo vya habari kuhusu ununuzi wa mitambo ya Dowans. Kampuni ya kimarekani ya Symbion Power yenye makao yake makuu Washington DC, leo imethibitisha kwamba imekwisha weka sahihi mkataba wa ununuzi wa mitambo hiyo iliyopo Ubungo Dar es Salaam.

Paul Hinks, Meneja Mtendaji wa Symbion amewaambia wanahabari sasa hivi katika hoteli ya Kilimanjaro Kempinski kuwa, “mazungumzo na Dowans yalikuwa ni magumu hasa ukizingatia historia ya mradi wenyewe. Kwa hiyo ilibidi kufanya uchunguzi wa kina kujiridhisha na kila kipengele cha makubaliano na pia ubora wa mitambo na tumejiridhisha kuwa mitambo hii iko katika hali nzuri ya matunzo”.

Hinks aliendelea kusema “nafarijika kusema kwamba sasa tumemaliza na kukamilisha mkataba wetu na Dowans na tupo tayari kuzalisha umeme hapa nchini. 120MW inaweza kusaidia kupunguza matatizo ya umeme hasa ukizingatia kuwa nchi inakabiliwa na tatizo kubwa la mgao wa umeme. Lakini, laiti kama TANESCO haitaafiki, tuna miradi mingi duniani ambayo inahitaji mitambo hii.
Mwasisi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Symbion Power LLC, Paul Hinks, akiongea na wanahabari sasa hivi hoteli ya Kilimanjaro Kempinski jijini Dar leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Symbion Power Africa, Balozi mstaafu Joseph Wilson
"Pamoja na ukweli kwamba tunauwezo wa kuitumia mitambo hii pengine duniani, Symbion inakusudia kupendekeza kwa TANESCO waridhie mitambo hii itumike hapa nchini. Mitambo hii imefanyiwa majaribio hivi karibuni na wataalamu wa kimataifa na imedhibitika kuwa iko katika hali nzuri sana na inaweza kuanza kutumika ndani ya muda mfupi sana kwa mategemeo ya kiwango cha hali ya juu", alisema.

Hinks pia kafafanua kwamba Symbion itashirikiana na kampuni ya Kimataifa ya kimarekani ya ProEnergy Services (PES) ambayo inauwezo na uzoefu mkubwa katika sekta ya umeme yenye makao yake makuu Missouri, Marekani. PES ambayo inajishughulisha na uzalishaji wa umeme sehemu mbalimbali duniani itakuwa ni mbia wa kutoa huduma ya uhandisi na uendeshaji wa mitambo.

Amesema Symbion Power tayari inauzoefu mkubwa katika miradi ya umeme ambayo inafadhiliwa na Serekali ya Marekani kama vile yale yaliyo chini ya Millenium Challenge Corporation. Symbion pia inashughulika na usambazaji wa umeme vijijini Tanzania inayojumuisha takriban kilometa 3,000 ya miundombinu ya kusambaza umeme.

Wakati huo huo, mwenyekiti wa Symbion Africa, Balozi mstaafu wa marekani katika nchi mbalimbali, Joe Wilson, alisema mitambo tuliyoinunua iliyoko Ubungo, imekaa bila kutumika takriban miaka mitatu sasa, wakati nchi imekuwa ikipata matatizo makubwa ya mgao wa umeme inayoleta changamoto katika uchumi wa nchi. Kwa niaba ya bodi ya wakurugenzi  ya Symbion, nasema tutafarijika ikiwa TANESCO itahitaji huduma kutoka kwetu”.

Symbion ni kampuni ya Kimarekani yenye makao yake makuu Washinton DC Marekani. - www.symbion-power.com


Ambassador Alfonso E. Lenhardt's Statement on Symbion Power Acquisition of the Power Plant in Ubungo

"We are pleased with the announcement that Symbion Power has decided to invest in Tanzania by acquiring a 112-megawatt power plant.  Energy is essential to support industry, agriculture, the education and health sectors, social services, and reliable water supply. The private sector will have an important role to play in providing long-term energy solutions in Tanzania.  We support the Ministry of Energy’s effort to attract investors and facilitate public-private partnerships. We encourage Tanzania to continue improving conditions for investment.  The United States actively promotes investment by American companies in Tanzania."

Ambassador Alfonso E. Lenhardt   

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 20, 2011

    this is a joke right???????kumbe do once imezimwa wakasingizia gas imefanya nini sjui ndo mana mgao....alafu wanatusaidia kulipa na lile deni ama?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 20, 2011

    Nahisi huu mgao unaoendelea ni kwa ajili ya kuwawekea mazingira mazuri hawa jamaa. It will soon be clear...

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 20, 2011

    "mambo ya siasa kwao hayana nafasi bali ni kazi tu na blah blah pembeni" - hii inafuraisha sana na kutia matumaini. Lakini wakumbushwe kuwa hizo zilizobatizwa 'siasa na blah blah' hapa bongo hazitazuilika iwapo kuna harufu yo yote ya ufisadi. Kama wamewnunua mzigo wa Dowans wakilijua hilo basi tunawakaribisha kwa mikono miwili. welkom to bongoland.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 20, 2011

    Wow! Finally, This is one of BREAKING NEWS I've been waiting for. For decades Tanzanians have being living in dark ages, now Americans will light up Tanzania. Symbion is among the biggest power producer in Arab countries now to Tanzania!! Hope this deal will move smoothly without political propagandas
    God bless The United States and God bless Tanzania and Tanesco.
    Great move for all individuals who made this deal possible
    Mdau, Houston TX.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 21, 2011

    Staff Vacancies

    SP/TZ/101 Regional Financial Controllers
    Project Location: Tanzania, East Africa
    Candidates must have a minimum of 5 years experience as a Financial Controller and recognized qualification as an accountant.
    Read full description >

    SP/TZ/102 Regional Construction Managers
    Project Location: Tanzania, East Africa
    Distribution line and substation managers with at least 10 years experience of project management in a power engineering construction company.
    Read full description >

    SP/TZ/103 Commercial Manager
    Project Location: Tanzania, East Africa
    20 years experience as a Quantity Surveyor with at least 5 years experience as Chief Quantity Surveyor or Commercial Manager.
    Read full description >

    SP/TZ/104 Distribution Line Supervisors
    Project Location: Tanzania, East Africa
    Wood pole distribution line supervisors who have at least 10 years experience...
    Read full description >

    SP/TZ/105 Substation Construction Engineers
    Project Location: Tanzania, East Africa
    Engineers with a recognized engineering degree who will supervise the erection and commissioning of 132kV and 33kV substations.
    Read full description >

    SP/TZ/107 Human Resources and Personnel Manager
    Project Location: Morogoro, Tanzania
    An HR Manager with 10 years experience in Tanzania dealing with a large labor force in excess of 1000 employees. Based in Morogoro. Must speak Swahili.
    Read full description >

    Wanted: Experienced People for Important Work
    Project Location: Africa and Middle East
    Position: Various
    Symbion Power is continuously seeking intelligent, ambitious, and experienced employees for its work delivering complex power engineering solutions to the world's developing nations.
    Read full description >

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...