Matangazo ya Zanzibar yakionyeshwa katika mechi ya ligi Kuu ya Marekani kati ya Seattle Sounders na na timu kutoka Arizona ambapo watazamaji zaidi ya elfu hamsini walihudhuria mechi hiyo huku watazamaji zaidi ya milioni ishirini waliona mechi hiyo katika TV.
Matangazo ya Mlima Kilimanaro yakiamba uwanja
Tangazo la kuvutia watalii wa Kimarekani watembelee Tanzania
Afisa wa Ubalozi wetu Washington DC Bw. Suleiman Saleh akikaribishwa kwa matarumbeta wakati ujumbe wa Tanzania ulipotembelea uwanja wa Seattle Sounders kuona jinsi tutavyoweza kujitangaza kwa watalii
Bw. Suleiman Saleh Afisa wa Ubalozi wa Tanzania Washington DC akiwa na Makamo Mwenyekiti wa Seattle Sounders/Seattle Hawks Bw. Lanz na Dk. Ezekiel Dembe wa Tanzania National Parks (TANAPA) wakati wa ziara hiyo.
Tanzania itapata nafasi hivi karibuni ya kutangazwa zaidi kiutalii nchini Marekani kufuatia mazungumzo yaliyoanza baina ya Serikali ya Tanzania na klabu ya soka ya Seattle Sounders ya Washington,Seattle ambayo pia inamiliki timu ya Seattle Hawks ya American Football.
Ujumbe wa Tanzania wa Bw. Ezekiel Dembe Ofisa kutoka Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Bw. Suleiman Saleh, Afisa wa Ubalozi wetu Washington DC umefanya mazungumzo na uongozi wa klabu maarufu ya soka ya Seattle Sounders na Seattle Seahawks ( American Football) ambazo wamiliki wake ni wamoja kuangalia uwezekano wa Tanzania kujitangaza kiutalii nchini Marekani, hususan kwenye michezo ya klabu hizo kubwa. Ujumbe ulifika katika dimba la Seattle Sounders wakati wa mechi yao ya ligi ya Marekani (MLS) walipocheza na Arizona na kushinda bao 1-0.
Ujumbe huo ulipokelewa kwa nderemo nje ya uwanja wa Seattle Sounders ambao kikundi cha matarumbeta kiliwatumbuiza, kabla ya wageni kwenda kushuhudia mandhari ya Uwanja wa Saunders ambapo watazamaji wapatao 50,000 walihudhuria mechi ya Saunders na watazamaji zaidi ya 60,000 walihudhuria mechi Sounders Sea Hawks ya American Football huku matangazo ya majaribio yakipamba mechi hizo kuitangaza Tanznaia na Zanzibar, ambapo tayari simu za ubalozini zimeanza kuigwa na Wamarekani kibao waliovutiwa na Tanzania na vivutio vyake.









Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...