Kata funika, piga ua, garagaza hapajapata kutokea mpishi hodar wa pilau na biriani kwenye shughuli kama Saidi Bajia ambaye ameanza shughuli hiyo takribani miaka arobaini iliyopita na hadi sasa hana dalili ya kupunguza spidi. Katika shughuli yoyote iliyo jijini Dar hukosi kumkuta Saidi Bajia akiwa katikati ya shaba akifanya mambo yake. Hivi sasa kuna takriban waishi wa aina yake 12 ambao ni wanafunzi wake na anana fahari kubwa kuwana wanashamiri.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 24 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 15, 2011

    Ok sawa ila jamani usafi mbele , hilo sufuria duh!

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 15, 2011

    michuzi kwanza lazima uzitizame maoni kisha uyaweke huyu jamaa anasema usafi sasa hiyo sufuria amepikiwa sasa vipi itakuwa safi?

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 15, 2011

    Hilo sufuria ndilo linalomfanya awike zaidi katika hayo mambo ya pilau na biliani.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 15, 2011

    Vipi Ali Mapilau?

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 15, 2011

    mafuta matupu..ndio maana magonjwa sugu yanaongezeka. Lakini afadhali sasa babu anatupatia tiba.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 15, 2011

    SUFULIA SIO CHAFU BALI IMECHAKAA TU. SASA ANZENI HARAMBEE ZA KUMNUNULIA SUFULIA MPYA, STOCK MARKET YAKE ITAONGEZEKA!

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 16, 2011

    BABU BAJIA ENDELEA.... USIKATE TAMAA KWA MASIMANGO ..... TAFUTA MRITHI MAANA HIVYO NI VIPAJI ADIMU.

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 16, 2011

    nyie nyote mliotoa maoni yenu ni mazuli sana kwamba huyo mpishi msimpe lawama kwanza sio mafuta wewe utachompelekea ndicho atacho kupikia wewe mwenyewe sawa kwa hiyo hana lawama pili sufuria yeye ktk mapishi yake kwanza hatumii jiko la umeme,hatumii pia jiko la gesi kwa hiyo jibu unalo mwenyewe ukiwa wewe mtanzania halisi (usiwe mtanzania feki)wa mambo ya magamba na sumu, ni mpishi mzuri na anae jali kazi yake kiwakati, pia asante mr.muhidin issa, kwamba na huyo mpishi anaalikwa mpaka kwenye hafla za taifa sema hamjui tu nyie wengine,freind junior, istanbul,TUR

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 16, 2011

    duh huyu mzee bado yu hai??? Allah akbar, lakini ALI MAPILAU noma pia

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 16, 2011

    Hicho chakula ni kimoto na sio rahisi kupata maradhi ya yanayosababishwa na uchafu. Pia biriani na pilau huwa inapikwa kwa kutumia viungo vingi (spices) ambazo huwa ni dawa pekee kama vile tangawizi, kitunguu maji na thomu, hiliki, mdalasini, uzile, pilipili manga. Pia huwa kuna salad nzuri ambayo hujaa vitunguu maji na malimau na ndimu. Ni chakula bora na kina kinga nyingi. Mdau CT, USA.

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 16, 2011

    Ali Mapilau mzee wa upanga ndo kiboko ya wapishi wa shughuli Dar nzima

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 16, 2011

    Saidi Bajia Anapatikana mitaa ya Rufiji na Nyamwezi Karikoo...Ukimuulizia Humkosi.... Jamaa Mashallah Msosi wake Lazima Ujirambe....Thanks Mdau Kwa Ku Post Picha hii,hakika nina ubao kinoma sasa especially biriani la TZ likipikwa na mtaalam kama saidi bajia...
    Houston,Tx

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 16, 2011

    yupo wapi huyu mzee details please

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 16, 2011

    michuzi huwa unaweka na kontact bwana , sasa tutampataje ?

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 16, 2011

    Kila kazi ina fani yake na taratibu zake:- kuhusu chakula/mlo Usafi ni
    misingi wa kutekeleza wadhifa huo. kwa hiyo kila kilicho usika na mapishi lazima liwe na kiwango ikubwa cha usafi usafi usafi hadi mwandalizi na mkaribishaji aandae kwa usafi.

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 16, 2011

    Hii pilau na biriani ikiwa sufuria limechakaa ndio linapika vizuri. Mbona mahotelini mafrying pen wanaonesha kwenye TV zile zilizochakaa ndizo zinazopika vizuri. Ulizani ma chef watawaambia. Huyo anayesema chafu kwao alikotoka vijijini sufuria au chungu cha ugari wa jana kinakoshwa leo ili upikwe ugari mwingine.

    Achane nao wapata leo, chips vumbi ndio chakula chao tarararara.
    Saidi Bajia tunamfagilia. Chakula cha kula watu 300 - 400 bila ya kumwita yeye mtakula ile pilau ya udongo mwekundu wanaopika ma-caterer wa mjini.

    Watuachie pilau na biriani yetu hata likiwa sufuria chafu wenyewe tunafaidi.

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 16, 2011

    huyu mzee anapatika mtaa wa muhoro na nyamwezi. kariakoo. wewe ulizia kwa saidi bajia tuu utaelekezwa. au fika msikiti wa makonde mtaa wa nyamwezi muulizie pale utaelekezwa. keep it up babu saidi

    ReplyDelete
  18. AnonymousMay 16, 2011

    MWANANYAMALA TUNA MTU ANAITWA JOLIJO NAE HAFAI KTK MAPISHI.....

    ReplyDelete
  19. AnonymousMay 16, 2011

    Heshima ma taadhima kwa SHEHE SAIDI huyu bwana ndiye alikuwa mpishi na msimamiaji wa shuguli ya harusi ya baba yangu ilofanyika tabora kabla ya miaka 30 ilopita na ni maarufu sana katika mikoa ya bara mwanza mpaka bukoba naukisafiri naye utastarehe maana hata na taarabu na sumsumiya anaimba

    ReplyDelete
  20. AnonymousMay 16, 2011

    Mdau wa May 16 09:21:00 AM 2011 Tarararara umenichekesha kweli! pilau nyekunduuuuu kama imetiwa dongo la kimasai! kwanza pilau raha yake utie viungo vizima vizima pilau wa kusaga viungo ya watu wa BARA A.K.A MRIMA huko wamepapia hawajui kupika pilau viungo vinasangwa nakwambia KARAHA TUPU ! kibaya viugno vya kusagwa kabisa havina harufu yote imeishia kwa muuza duka ! watuachie wenyewe hiyo pilau babu! Saidi Bajia kaza mdundo! na mwengine Mzee Ali Mapilau wa Tambaza pale mtaa wa Mindu nae MAshaALLAh hajambo !

    Haya Kaka Michuzi Ahsante!

    ReplyDelete
  21. AnonymousMay 16, 2011

    nadhani hiyo siyo pilau watu hajaiangalia vizuri hiyo ni jama rost iliyochonganywa na viazi inarangi safi sana asante kaka michuzi kwa kuposti hii wengine tunashiba kwa macho

    ReplyDelete
  22. AnonymousMay 16, 2011

    Watu wengine biriani wanaiona kwenye sinia imeshapakuliwa. Hapo ukimpata Saidi umkabidhi mchele wa basmati halafu unampa na ration yako (asilimia ya mchele na nyama) ukiipiga 50-50 inakua ndio mambo tonge nyama.

    ReplyDelete
  23. AnonymousMay 20, 2011

    Ankal, nimemtafuta Said Bajia sanaa. Naomba contact zake nina shughuli June. pleasee.

    Cate

    ReplyDelete
  24. ahmed said bajuaFebruary 22, 2016

    Asalam aleykum vp hali zenu jamani nashukuruni sana kwa kujai kazi yangu tupo KARIAKOO mtaa wa MUHORO ST NA CONGO na karibu na msikiti wa makonde na tunapokea oda mbalimbali mnakaribishwa sana
    napatikana kwa namba zifuatazo
    0654 215213
    0658 358661
    0784 358661
    AHSANTENI SANA NA NAWATAKIA KILA LA KHERI

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...