Ja Rule akiwa amezingirwa na wafanyakazi wa
88.4 Clouds FM radio alipotembela Tanzania mwaka 2006

Msanii wa Hip-hop  Ja Rule yuko lupango ambako alijipeleka mwenyewe katika gereza moja huko New York, Marekani, na  kuanza kutumikia adhabu ya kuwa kifungoni kwa miaka miwili.
Rapa huyu ambaye ameshafanya ziara Tanzania wakati wa Fiesta ya mwaka 2006, na ambaye jina lake halisi ni  Jeffrey Atkins,  alikiri makosa mwezi Desemba mwaka jana kwa kukutwa na silaha kinyume cha sheria ndani ya gariu lake la kifahari, huku silaha hiyo ikikutwa imekwanguliwa namba zake za usajili. Tukio hilo lilitokea  kitongoji cha New York cha  Upper West Side mnamo July mwaka 2007.
Ja Rule alijisalimisha mwenyewe gerezani hapo saa nne asubuhi siku ya Jumatano, kabla ya kupelekwa  Rikers Island, ambako atapangiwa gereza atalokwenda kutumikia adhabu hiyo.
Katika miezi ya karibuni Ja Rule alikuwa anamalizia kurekodi albamu yake  mpya – ya kwanza katika miaka sita – inayotegemewa kuwa sokoni baadaye mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...