Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi Profesa akishuka kwenye trekta maalumu baada ya kuliendesha linalofanya kazi ya kuandaa mashamba kwa kwa utaalamu wa kisasa, trekta hilo lina vifaa vinavyoweza kuweka udongo ukawa katika hali ya usawa na ukawa bila na aina yoyote ya mabonde
Profesa Anna Tibaijuka akisikiliza kwa makini maelezo ya namna kiwanda cha sukari cha Kagera kinavyoandaa mashamba kwa kutumia utaalamu wa kisasa kwa njia ya satellite.
Balozi wa jumuia ya nchi za ulaya nchini Tanzania Tim Clarke (aliyevaa kofia) akionyeshwa sehemu ya maji ya mto Kagera ambapo kiwanda cha Sukari Kagera kimefunga mtambo wa kusukuma maji yanayomwagililia mashamba ya miwa yenye ukubwa wa hekta 4,000.
Balozi wa jumuia ya nchi za ulaya nchini Tim Clarke (mwenye kofia)akipewa maelezo wakati akionyeshwa mashine ya kumwagilia miwa maji, mwingine anayesikiliza kwa makini ni waziri wa ardhi, nyumba na makazi Profesa Anna Tibaijuka. Picha na Audax Mutiganzi wa Globu ya Jamii, Misenyi






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...