Mgeni Rasmi katika ufunguzi wa Tamasha la Filamu Zanzibar (Zanzibar Film Festivar),Waziri wa Utawala Bora,Mh. Mathias Chikawe akitoa hotuba fupi katika ufunguzi huo unaoendelea hivi sasa ndani ya viwanja vya Ngome Kongwe,Zanzibar.Waziri Chikawe amewataka Wazanzibar na Watanzania kwa ujumla kuendelea kuyaenzi matamasha mbali mbali yanayofanyika katika visiwani hapa.
Mwenyeketi wa Bodi wa Tamasha la Filamu Zanzibar,Hassan Mitawi akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika muda mfupi uliopita katika viwanja vya Ngome Kongwe Zanzibar usiku huu.
Mkurugenzi wa Tamasha la Filamu Zanzibar (ZIFF),Prof. Martin Mhando akitoa maelezo mafupi ya Tamasha hilo ambayo yamezinduliwa rasmi usiku huu ndani ya viwanja vya Ngome Kongwe,Zanzibar.
Washehereshaji wa Ufunguzi wa Tamasha la Filamu Zanzibar (ZIFF),Haz T pamoja na Amanda wakiwajibika usiku huu.
Mgeni Rasmi katika ufunguzi wa Tamasha la Filamu Zanzibar (Zanzibar Film Festivar),Waziri wa Utawala Bora,Mh. Mathias Chikawe (kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Tamasha la Filamu Zanzibar,Hassan Mitawi pamoja na Mkurugenzi wa Tamasha hilo,Prof. Martin Mhando ndani ya viwanja vya Ngome Kongwe,Zanzibar usiku huu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...