KUNANI TRA IDARA YA KULIPIA MAGARI YANAYOINGIA???

Mimi ni Mtanzania ambaye nafanya kazi kwenye taasisi moja hapa nchini. Baada ya kujibana sana niliweza kuagiza gari na limefika. Kwa muda wa siku kadhaa sasa najitihada za wakala wangu hadi sasa sijui kinachoendelea, lakini nyepesinyepesi ni kuwa TRA wamebadilisha system yaulipiaji magari ambayo ndiyo imesababisha huu usumbufu.

Mimi kamaMtanzania, najiuliza je TRA, inayohitaji kukusanya mapato mengi ilikutukomboa kwenye umaskini inakatisha tamaa walipaji kodi kwa ucheleweshaji wa makusudi!. 

Hivi TRA ina muda wa kikomo wautoaji huduma (service level), hivi TRA lini itatilia maanani huduma bora kwa wateja?  Hivi ni lini TRA wajivunia kutoa huduma bora kwa muda mfupi au muda sio jambo wanalojali? Ucheleshaji huu unaongeza storage cost ambazo bandari inatoza kwa kila siku gari linapokaa!.

Natumaini blogu yajamii ni njia bora ya kuliweka 
hili wazi na tukipata ufafanuzi wa TRA utaleta ahueni.
Mdau Kigamboni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 10, 2011

    aise we acha tu nna wiki 2 naambiwa system znafungwa huku bandari wanaesabu storage na garama ziko juu ukilinganisha dolla ilivo sasaivi inasikitisha sana maisha ya mtanzania yanazidi kuwa magumu kila siku ushuru pia umepanda maradufu

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 10, 2011

    yaan kaka pole tra hizo ndio zao hamna watu wa rushwa kama hao bila pesa gari halitoki watakwambia makaratasi hayaja pita bado oh namany more lakin ukiwapa pesa tu gari utatoa dakika so just wape pesa ya moto .watu wote wanao toa magari wawe wanawapa pesa ya moto hapo ndio wataacha kuchukua rushwa.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 10, 2011

    Wewe unayesapoti rushwa una mawazo finyu kweli kweli. au unafanya kazi TRA? Haki haipatikani kirahisi. Mkiwapa rushwa ndio mnawafanya waone huo ni utamaduni wao hivyo asiye na pesa hatapitishiwa gari lake. Vumilia tu kaka.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 10, 2011

    Mimi lakini nilitoa gari pale mara mbili kupitia kwa agent wangu haikunichukua muda mrefu. gari ya kwanza ilinichukua kama siku nne tangu iingie bandarini ambapo ya pili ilinichukua kama wiki moja.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 10, 2011

    Michuzi tunashukuru ulivyobadilisha utaratibu wa kuingiza maoni na kutuma. Sasa hivi ni rahisi sana na meseji inakwenda kiurahisi. Yaani umetuchanulia sisi kazi yetu ni kuingiza tu na kutuma.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 10, 2011

    kwa kweli TRA wamezidi sana ni mateso makubwa kutoa gari utasubiri release mpaka uchoke ila ukitoa tu pesa basi mambo shwari

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 10, 2011

    tra wamekuwa miungu watu mbona mamlaka nyingine husika kama ticts , bandari,icd's na cfs hawana usumbufu kama wao? wabadilike mimi naamini ukiwepo usimamiz mzuri ipo kodi ya kutosha ukizingatia nchi zaid ya tano wanapitisha karibu kila kitu pale dar na uchumi wao wakua why not us tuwe strategic kwamba hii gate way ya nchi zote hizo itumiwe vizuri kukuza uchumi wahusika mnajua lakini sijui inakuwaje!

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 10, 2011

    bora watu waendelee kutoa rushwa tuu ndio short cut

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 10, 2011

    TRA Fanyeni kazi yenu kwa mujibu wa sheria mambo mengine achaneni nayo

    David V

    ReplyDelete
  10. Hii ya kutoa maoni kwa mtindo huu iko sawa kaka Michuzi hapo timeelewana!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 10, 2011

    Ndio maana Mheshimiwa Mkapa alitimua kazi wote. Nyie hamuoni maisha wanayoishi mitaani. Ni rushwa kuanzia hizo ndogo na mpaka kubwa. Tusiseme mengi ila hao ndio wenye hii nchi. Wananitia hasira sana. Hivi ni nchi zote ukifanya kazi TRA basi wewe unakuwa na gunia la fedha chumbani. Maana nasikia wanaogopa benki watakamatwa na PCCB. No wonder tutakuwa masikini milele

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 11, 2011

    Testing uharaka wa maoni kupostiwa hapa

    ReplyDelete
  13. Hahahahaaaa mdau umenifurahisha kweli. Kwa taarifa yako wewe na wadau wapendwa wengine ni kwamba Globu ya Jamii hailali, timu ina shifti nne za 24/7 nadhani umejionea mwenyewe na hiyo 'testing yako'

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 11, 2011

    Hahahahhh
    Ni nadra sana Ankal kuandika maoni, ahsante sana. Tunashukuru kama unazingatia maoni yetu, sisi ndo wamiliki haswa wa globu. We are why you blog! Big up sana Ankal

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...