Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kagera Henry Salewi akiongea  na waandishi wa habari kwenye ukumbi wake wa mkutano. Kawaeleza  waandishi waandike habari za kuielimisha jamii iachane na tabia ya kujichukulia sheria mikononi ya kuwasurubu wale wote wanaotuhumiwa kwa kujihusisha na makosa mbalimbali, tabia ambayo Kamanda amesema imekithiri mkoani Kagera na kuna haja ya kuirekebisha. picha na Audax Mutiganzi wa Globu ya Jamii, Kagera

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 20, 2011

    hahaha slow news day...ebu nitafutie kamanda wa polisi asiyekerwa na watu kujichukulia sheria mkononi...nothing new here!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 20, 2011

    Mi napenda sana wananchi wanavyojichukulia sheria maana polisi, mahakama hawana haki unampeleka mtuhumiwa anakurudia kesho kukuua. Sasa faida iko wapi? Tanzania kesi za uongo ni nyingi kuliko hata waliotenda kweli so what is the point? To kill them is real solution because we gonna reduce the population in magereza

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 20, 2011

    yaani wee wewe anony wa tar 20 July saa 09:46 PM hujui usemalo. hao jamaa wanajichukulia sheria mkononi hawajui haki. mimi nawaita wapumbavu. samahani kwa kutumia neno kali lakini ndo wanachostahili. mfano juzi tu kuna mtu kaibiwa ba kakatwa mapaga mida ya usiku wa saa sita kwa maelezo yake. akasema aliyemkata mapanga na kumwibia ni fulani. kwamba aliweza kumtambua kwa jaketi alilovaa. wananchi kwa huo upumbavu wao wakakurupuka na kutaka kumuua mtajwa. hawakujiridhisha kwa namna yoyote kuhusika kwa mtu huyo. walishinwa kuangaia kama angalau kuna matone ya damu kwenye jaketi au limefuliwa,lakini waliamua kuua.

    naomba hali kama hiyo imkute nduguyo au wewe ndo ujue maana ya kujichukulia sheriamkononi. kwani unaweza kuwa na visa na mtu, akipatwa na tatizo anakutaja wewe. kwa vile hakuna shera wala haki unauawa au nduguo anauawa ndo ujue usemalo.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 20, 2011

    bila kuwaadhibu hawataacha hiyo tabia. kamata wahisika wawe mfano. utaona kamaitatokea tena. maneno tu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...