Na Madaraka Nyerere, Butiama

Miezi michache iliyopita nilipokea barua pepe kutoka Bulgaria ikiniarifu kuwa kuna Mtanzania anaitwa Mohamed Sakara aliyedhaniwa amekufa lakini ilibainika kuwa yu hai na habari zake zikaandikwa kwenye gazeti moja la huko Bulgaria. 
Mohamed Sakara alivyo leo

Picha za hivi karibuni za Mohamed Sakara, akiwa jijini Sophia, nchini Bulgaria.
Raia wa Bulgaria aliyesoma hizo habari aliniandikia barua pepe kuniomba nijaribu kuwatafuta ndugu zake Sakara huku Tanzania. Nilituma hizo taarifa kwa mwanablogu Muhidini Michuzi lakini sina hakika kama zilitoka kwenye blogu yake.

Kwa kifupi Sakara alienda nchini Bulgaria kwenye miaka ya 1980 kusomea uhandisi, lakini hali ilimuendea vibaya mpaka kujikuta hana uwezo kabisa wa fedha na akiishi kwa shida mitaani. Angependa kurudi Tanzania lakini hana uwezo wa kujilipia nauli. Inasemekana baada ya kutangazwa amekufa, ndugu zake hawakuendelea kumtafuta, lakini ukweli ni kuwa yuko hai. Taarifa zake nyingine ni:
  • Amezaliwa mwaka 1961
  • Inakisiwa alisoma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kati ya mwaka 1982 - 1984 halafu akaenda Bulgaria ambako alikuwepo mpaka kipindi napata taarifa hizi
  • Anatoka kwenye familia ya watoto 8
  • Taarifa za kaka yake Abeid Hassan Sakara ni: amezaliwa mwaka 1954; ameandika kitabu "Jizoeze Kiswahili", na "Rashid Mfaume Kawawa"; alikuwa mkuu wa kitengo cha uchapishaji cha Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (Dar es Salaam); alikuwa akiishi Upanga Mashariki, Mtaa wa Maweni, Na.244, lakini hajulikani alipo kwa sasa.
Yoyote anayemfahamu Mohamed Sakara au ndugu zake awasiliane na mimi ili nimpe anwani ya aliyenitumia taarifa hizi toka Bulgaria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 21 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 04, 2011

    habari, nafahamu baadhi ya ndugu zake, nawajulisha hapa,so watawasiliana nawe kwa njia ipi?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 04, 2011

    pole sana bwana sakara, ila ni kweli kabisa wabongo kibao ni mahomeless nchi za watu, jamani majuu sio alimradi tuu lazima upambane haswa vinginevyo unakuwa homeless live haijalishi umesoma au hujasoma.
    wengine kutwa kupiga wenzao mizinga kila kukicha bora liende, ni hatari.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 04, 2011

    Mohammed Sakara mambo yameenda kombo, lakini hiyo hata bongo ingemkuta maana inaonyesha kuwa ni mtu "homeless". Cha kufanya sasa ndugu Mohammed ni utafute "immigration lawyer" akutetee ili upate uraia wa Bulgaria maana umeishi huko zaidi ya robo karne. 2012 Bulgaria inakuwa mwanachama kamili wa EU hivyo ukiwa na uraia wa Bulgaria mambo yako yatakuwa mazuri na utaweza kuja UK na kubeba boksi ili upate fedha kidogo za kuanza maisha hapo Bulgaria au hata UK. Kurudi bongo hafla sio vizuri.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 04, 2011

    Je ana undugu na Marehemu Fatuma Sakara aliyekuwa Diwani wa Upanga Mashariki?

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 04, 2011

    hilo ni jukumu la serikali au balozi zake kuregesha raiaa wake nyumbani.mdau hapo juu unaesema eti bulgaria aombe uraiaa huezi kumsaidia kitu maana huko njaa kali bulgaria.hungary,poland,latvia hizo nchi za eastern europa balaaa.wazawa wahuko wanakukimbia pia nakuzamia western europa

    ReplyDelete
  6. Sio hatufutiwe nauli miaka yote aliyoishi Bulgalia sio mchezo jamani.Muhimu ni mawasiliano sio kumrudisha kwao HAKI YA BINADAMU Ulaya kuna watu wanaishi hivyo,sio kucheka au kulaumu ndio maana nchi zilizoendelea zinawasaidia raia wake.Hapo kwenye picha anakula fish and chips na bia je?akirudi TZ hataweza kula hivo?Hatujui alihamua vipi mpaka akaishi hivyo,chukulia barafu je?anaishije huyo?
    Kumrudisha huyo TZ ni sawa na matonya kumridisha Dodoma mwacheni aendelee na maisha ya watu wasiofikili cha kesho wao wanawaza kula na kunywa nampa hongera huyo jamaa kwa kuishi nchi hiyo kwa muda mrefu haaa

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 04, 2011

    yeah,marehemu Fatuma Sakara ndo aliyekuwa mke wa huyo kaka yake Abeid Sakara

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 04, 2011

    Inasikitisha sana
    Ilikuwaje mwananchi huyu kufika katika hali hiyo ikiwa yasemekana kuwa ana elimu ya chuo kikuu DSM, sasa yeye ni kama mheshimiwa Matonya.
    Mtu amshike mkono amuongoze kwenye ubalozi wa nchi, and they are duty bound to repatriate him back to Bongo

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 04, 2011

    Inasikitisha kwa kweli ukizingatia alikuwa msomi wakati anaenda huko Bulgaria. Kisomo chake kingeweza kumsaidia. Lakini hii inaonyesha pia uhalisi wa maisha kwa nchi za wenzetu kama hizi ambako utaifa unapewa priority kwenye kazi. Utasoma na ma-degree yako lakini ikifika kwenye kuomba kazi hakuna anaekuangalia kwa vile wewe ni immigrant. Bila shaka state aliyo nayo imetokana na msongo wa mawazo na neglect ya muda mrefu. So sad, angebaki Tanzania, bila shaka ingekuwa quite a different and a promising story.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 04, 2011

    Jamani msimkedhehi mwenzenu.We bwana nyerere ni mbulgaria gani amekuandikia? Mbona mnatafuta sifa kwa kutumia maafa ya wenzenu? Njia ya kupata habari kamili haswa kuhusu sakara ni kupitia blog au facebook group BULGARO.

    mdau KILI
    kjmalisa@abv.bg
    bulgaria

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 04, 2011

    MIMI SISHANGAHI HATA INDIA WAPO WENGI WATAZANIA WANAFANYA KAZI YA UMATONYA. NA SEREKALI YETU INAJUA KUWA KUNA WATU KAMA HAO NA AWASAIDII.
    WATANZANIA KWELI HATUJALI MTU ZAIDI NA YULE UNAYEMJUA
    MDAU CHINA

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 04, 2011

    Bulgaria kuna wanageria wengi tu na wanamaisha mazuri kwani wanasomesha kiingereza na kutafsiri magazeti kwa kiingereza. Ndugu yangu Mohammed inaonyesha anamatatizo ya kukata tamaa hivyo cha msingi ni kuwa apate kwanza matibabu ya maradhi yanaitwa "Depression". Maana yamemkumba kwa muda mrefu sasa.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 04, 2011

    Wahusika msaidieni yaliyomtokea yametokea siku zote binadamu tunaanguka na kusimama tena kila la kheri mzee wetu Utapata msaada tu

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 04, 2011

    I think as someone said above, this mwananchi has mental health problems and needs to be brought back home.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 04, 2011

    Kazi mojawapo ya balozi wa Tz huko ni kumsaidia Mtz, hawezi ajiuzulu, maana wanajisahau inakuweje Mtz awe matonya kwenye nchi za watu na mabalozi wao wapo? Kila mtu huwa anakosea na Watzwengi wakifika nje hawana umoja na kama ni miaka hiyo ndo kabisa na tena wengi wanajifanya wanajua kila kitu. Wakati binadamu huwezi kujua kila kitu.
    Anyway inaelekea yuko resedential home. But labda akipelekwa home atakuwa fine. But ni vyema kujua kwanza atafikia wapi na afya yake ikoje before maana nchi za wenzetu haki za binadamu zinazingatiwa kuliko Tz iliyopata uhuru MIAKA 50 ILIYOPITA. Mhhh inatisha. Pole kaka

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 04, 2011

    MASIKI BAB WA WATU SIJUI NINI KILIMKUMBA MMUNGU AMPE FAHAMU AJITAMBUE AWE MTU KATI YA WATU NA KISOMO CHAKE ALAFU NI MTU MZIMA NASIKIA UCHUNGU SANA HADI MACHOZI YAMENITOKA

    SIE KAMA WATANZANIA TUNA MSAIDIAJE HUYU MTU JAMANI? HASA WALE WANAO KAA BULGARIA MTU HUYU ANAONEKANA AMESHAATHIRKA KIAKILI KUTOKANA NA MAISHA

    SIMLAUMU WALA KUMDHIHAKI KAMWE SITOFANYA KWANI BINAADAMU HATUWEZI KUJIJUA TUNAKO KWENDA WISH NINGEKUWA BULGARIA NINGEJARIBU VILE NAWEZA

    TAFADHALINI SANA WATU MNAOKAA HUKO MUMSAIDIE KWANZA MZEE WETU KWA KILA MALI M MUNGU ATAWALIPA HAMUWEZI KUJUA NINI KILISABABISHA AKAWA HIVYO NCHI ZA WATU KUNA MENGI

    MICHUZI TAFADHALI SANA FANYA CHANGAMOTO ZOZOTE TUMSAIDIE MZEE HUYU M MUNGU ATAKULIPA JAZA YAKO HUWEZI JUA MANGAPI AMEYAPITIA MZEE HUYU TAFADHALI SANA

    YABINTY NALIA KWA SIMANZI

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 05, 2011

    hapa nilipo ninona uchungu sana mpaka machozi yananitoka na simfaham huyu bwana. angekua ni mamerika yuko abroad na akajikuta kwenye hali aliyonayo serikali yake ingemrudisha nyimbani haraka sana. watanzania na ubalozi wa tanzania wamsaidie arudi nyumbani. hata kama ubalozo hauna pesa watanzania tulioko nje na popote kule tumchangie.

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 05, 2011

    Pole sana kaka Sakara. Hata hapa Reading yupo mtanzania mwenzetu aitwaye Zinga, kwa wale wanaomfahamu hali yake ni mbaya zaidi kiasi kwamba hawezi kuomba kutafutiwa ndugu zake. Naamini Zinga akifanikiwa kurudi nyumbani Tanga atapatiwa ufumbuzi wa matatizo yake ya kiafya pia.

    ReplyDelete
  19. Mtanazania aliyemaliza masomo Bulgaria.July 25, 2011

    Namfahamu sakara .tulisoma nae bularia maisha yake yalikuwa ya anasa na alikuwa hakai hosteli alikuwa anakaa apartimenti ya kukodi na mama wa Kibulgaria. Huwa alikuwa akisafiri Sweeden na uingereza wakati wa likizo.mambo yake yalikuwa safi, lakini masomo yalikuwa yanamwendea kombo. watanzania wengi walirudishwa kwa msaada wa UN, yeye alikuwa wapi? mbona akina Sindeu Mchau, chesko , Dr. Omari wapo SOFIA je wanaishije hao? inaelekea huenda sakara ana Ugonjwa wa akili. Nakuomba ndugu michuzi Uwasiliane na wizara ya Elimu elimu ya juu( muone mama Kibaya) atasaidia Bwana sakarsa arudishwe Bongo kwa kushirikiana Na wizara ya elimu Bulgaria. pia Balozi wa tanzania Moscow ajulishwe( wasiliana na wizara ya mambo ya Nje).Kama Sakara amesalimu amri na kuamua kurudi Bongo msaidie hivyo. ni jukumu la serikali ya Tanzania kuhakikisha kuwa anarudi tanzania haraka sana.naomba Tangazo hili ziwekwe katika daily news na ikiwezekana uundwe mfuko au akaunti tumchangie ndugu yetu sakara. Bulgaria ni wanyanyasaji sana angalia jino moja wameshamng'oa inasikitisha sana. Pole sana sakara

    ReplyDelete
  20. Nashukuru kwa aliyeweka taarifa hizi kwenye blog. Nilichelewa kuiona ila huyu Bwana nimesoma nae Azania. Alikuwa na akili sana kiasi cha kuwa mwanafunzi bora alipomaliza form IV akiwa na A nane. Pia alisoma A level Azania na licha ya kutokuwa na walimu kwa vipindi tofauti alifaulu sana akiwa daraja la kwanza la point 6. Baada ya JKT aliingia Chuo Kikuu kuchukua uhandisi ila akiwa mwaka wa pili kuingia wa tatu aliamua kwenda Bulgaria. Ukweli tulimshauri lakini hakushaurika. Yaliyotokea huko Bulgaria ni pamoja na kutokuhudhuria vipindi akiendekeza Starehe na Biashara. Yaliyopita si ndwele tugange yaliyopo. Je kuna utaratibu wowote wa kumchangia ili arudi hapa nchini. Pia kwa tabia yake ninavyomfahamu inabidi akubali kwanza kwa vile ni mbishi sana kwa jambo analoliamini kuwa ni sahihi kwake.

    ReplyDelete
  21. Nashukuru sana kwa habari hizi, huyu ni mjomba wangu.

    We have been trying to reach him for years. Please Please if you do have any updates with regards to where we might be able to find him, please let me know.
    I have just come across this blog today, when I was doing my little research, and I am hoping it is not too late(2016).

    I can be reached through iqbasetn@gmail.com or 9132020285 USA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...