Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya ndege ya Precision Air Michael  Shirima akitoa maelezo wakati wa uzinduzi wa safari ya kwanza  ya Ndege ya kampuni hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 111, ambayo imeanza safari yake kati ya Dar es Salaam kwenda Johannesburg  Afrika Kusini wakati wa hafla hiyo iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jana.Kulia ni Mkurugenzi Mkuu na Meneja Mwendeshaji wa Precision Air Alfonse Kioko na (Kushoto) Mkurugenzi wa TCAA John Njawa.  
 Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya ndege ya Precision Air Michael  Shirima akitoa maelezo wakati wa uzinduzi wa safari ya kwanza  ya Ndege ya kampuni hiyo 
 Baadhi ya abiria wakisubiri kusafiri na Ndege nambari PW 700.Boeing 737-300 ya Shirika la ndege la Precision Air ambayo ilizindua safari yake jana kati ya Dar es Salaam kwenda Johannesburg Afrika Kusini, kwa promosheni ya Dola 57 ili kuwawezesha watu wengi kusafri na shirika hilo
 Baadhi ya Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali nchini  wakisubiri  kusafiri na Ndege nambari  PW 700 Boeing 737-300 ya Shirika la ndege la Precision Air ambayo ilizindua safari yake ya kwenda Johannesburg Afrika Kusini jana kwa promosheni ya Dola 57 ili kuwawezesha watu wengi kusafiri na shirika hilo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Ndege la Precision Air Michael Shirima wa pili kushoto, Mkurugenzi wa TCAA John Njawa, Mkurugenzi wa Huduma za Uchukuzi, Wizara ya Uchukuzi, William Nshama (kulia) na Mkurugenzi wa Biashara Phill Mwakitawa wakijadilia  jambo katika hafla ya uzinduzi wa safari ya ndege ya Precision Air  kwenda Johannesburg Afrika Kusini kwa promosheni ya Dola 57.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Precision Air oyeeee! mko juu...
    i msafiri

    ReplyDelete
  2. habari njema!!!! ila rekebisheni website yenu inaboa pale unapotafuta kubook flight ipo very slow na muweke ratiba ya J'bourg trips tujue lini katika wiki kuna ndege.

    ReplyDelete
  3. me cjaelewa ni dola 57 au dola 570 nisaidieni kidogo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...