Asalaam aleykum, Ramadhan Maqbul

Ningependa kuwafahamisha kuwa Google ambayo inamiliki youtube kwa kushirikiana na wizara ya Habari na Utamaduni ya Saudi Arabia kuonyesha Ibada zote live toka Makkah. Hii ni mara ya kwanza kwa ushirikiano huo na hii inawapa nafasi waislam na wasio waislam wakifanya ibada katika msikiti mkuu wa Makkah.

Kwa wasio jua ni kuwa hiyo nyumba ambayo waumini  wanazunguka  inaitwa Kaaba na ilijengwa na nabii Ibrahim (Abraham) na mwanae Ismael (Eshmael)  na wanaibada wanatakiwa kuizunguka mara saba huku wakimwomba Mwenyezi Mungu  kama tulivyoamrishwa.

Tazama ibada live hapa:


Pia ningependa kuwapa link ya watu wanaotaka kusikiliza Qur'an online toka kwa wasomaji mbali mbali kama akina Abdelbasitm Shurain na wengineo...unaweza kusiliza hapa:


Mwisho naomba tuendeleze ibada zaidi katika hili kumi la mwisho na pia msisahau kutoa Zakatul Fitri mapema kwa wasio jiweza na hasa yatima na wengineo

wako katika uislam

Muyaka wa Kisarawe

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Shukran sana mdau

    Naomba michuzi uiache hii juu kwenye siku mbili tatu zilizobaki ili na wengine wapate fungu lao kwa kusoma na kusikiliza

    ReplyDelete
  2. Jazaak lwah,mungu akuzidishie brother kwa kutupa habari njema kama hizi.

    RAJABU.

    ReplyDelete
  3. Manshallah
    I have spent long periods just watching the live stream and listening to quraan
    Allah yebarik

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...