Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Balozi Fulgence Kazaura akimtunuku PhD Waziri wa ujenzi Dk. John Magufuli katika mahafali iliyopita ya Chuo Kikuu hicho

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Balozi Fulgence Kazaura kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kipindi kingine cha miaka minne.


Taarifa iliyotolewa leo, Jumanne, Oktoba 18, 2011, na Katibu Mkuu Kiongozi Phillemon Luhanjo imesema kuwa uteuzi huo unaanza mara moja leo hii.


Balozi Kazaura alikuwa Mkuu wa Chuo hicho katika kipindi kilichopita kilichoishia Julai, mwaka huu, 2011.


Imetolewa na:


Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.


18 Oktoba, 2011

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...