
Askofu Charles Gadi wa Goodnews for All Ministry (aliyeinua mkono),akiwaongoza wachungaji mbalimbali, kuombea mvua kwa kuimwagia maji ramani ya Tanzania, kutumia kifaa maalum, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Biafra jijini Dar es Salaam


Africa will never cease to amaze me... "Kifaa maalum", tunaomba ufafanuzi zaidi kuhusu hiki kifaa na data za jinsi kinavyoweza kuleta mvua. Tumieni nguvu zenu kuhamasisha kulinda misitu yetu na vyanzo vya maji, hapo mtakuwa kweli mmeomba mvua inyeshe.
ReplyDeleteama kweli usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Na siri ya mtungini aijuae kata.
ReplyDeletehaya. na hawa watu wako serious hapo ujue?
ReplyDelete= = =
Buffalo,
New York
jamani hivi kwa nini wasiwaombee mafundi wa mitambo ya richmond wajaliwe ujuzi zaidi ili tatizo la kuzima zima umeme liishe??? maana mvua hata ikija saa nyingine inazidi inaleta na mafuriko..sasa ikizidi ikaleta na mafuriko nani atafidia hasara..waombaji ama waombewa....??? jamani tuwe tunaomba tunataja na ukubwa wa tatizo ama sivyoooo...??? mhhhhhh
ReplyDeleteKama alivyosema mchangiaji hapo juu kuwa hamasisheni waumini wenu walinde vyanzo vya misitu, wasikate miti ovyo.
ReplyDeleteMimi nadhani nyie viongozi wa dini mnaenda shule na mnasomea mambo mbali mbali nadhani hata elimu ya mazingira pia. La msingi hamasisheni waumini wasikate miti kabla ya kupunda hapo ndo nitawaelewa ila hayo maombi yenu hayafiki popote.
Ni sawa na ukiwa unaumwa halafu huendi hospitalini unajidai neno linaponya, hapo ndugu utakufa bila ``madrip``.
Hii safi
ReplyDelete