Waziri Mkuu Mstaafu Mh Cleopa David Msuya akimpa pole Balozi
Juma Volter Mwapachu kwa  kufiwa na  mwanae, Harith
 Waziri Mkuu Mstaafu Mzee Cleopa David Msuya akisaini kitabu cha rambirambi ya kufariki kwa Harith Mwapachu, mtoto wa Balozi Juma Volter Mwapachu (kulia) nyumbani wa wafiwa Mikocheni jijini Dar.
Karibu yake ni kaka wa Balozi, Mh. Bakari Mwapachu akifuatiwa na Mzee Hashim Mbita
 Balozi Juma Volter Mwapachu akipewa pole na marafiki zake waliokwenda kumpa pole msibani
 Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Mbowe akipokewa na Dkt Hellen Otaru  alipowasili msibani
 Balozi Juma Volter Mwapachu akifarijiwa na Mh Freeman Mbowe
 Mh Bakari Harith Mwapachu akiongea na Mzee Hashim Mbita (kulia) na Mh Freeman Mbowe msibani
Waziri Mkuu Mstaafu Mzee Cleopa David Msuya akiweka saini katikam kitabu cha maombolezo hapo msibani
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika Kitabu cha maombolezo cha Harith Mwapachu, ambaye ni mtoto wa Juma Mwapachu, aliyefariki dunia leo asubuhi.Kulia ni Balozi Juma Mwapachu.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na mke wa Balozi Juma Mwapachu, Rose Mwapachu, wakati alipofika nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam leo jioni kumpa pole kufuatia kifo cha mtoto wake, Harith Mwapachu kilichotokea leo asubuhi
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha CHADEMA Freeman Mbowe, wakati walipokutana katika msiba wa mtoto wa Balozi Juma Mwapachu, Harith Mwapachu nyumbani kwa Mwapachu Mikocheni jijini Dar es Salaam leo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya waombolezaji, wakati akiondoka nyumbani kwa Balozi Juma Mwapachu, wakati alipofika kutoa pole kufuatia kifo cha mtoto wa Balozi Juma Mwapachu, Harith Mwapachu leo Oktoba 11. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. mUngu amrehemu,is that Harith who we went to Arusha School with,mdogo wake Hamza?....anybody?

    ReplyDelete
  2. R I P HARITH.MOLA AWAPE NGUVU WAFIWA KUKABILIANA NA FARADHI ALIYOIPATA MWENZETU.

    ReplyDelete
  3. May His Soul Rest In Peace,

    ReplyDelete
  4. MAY THE SOUL OF HARITH MWAPACHU REST IN PEACE

    ReplyDelete
  5. Inna lillah wa inna ilayhirajiuna

    ReplyDelete
  6. Anonymous wa kwanza, ndio Harith unaemsema, hatunaye duniani. RIP Harith

    ReplyDelete
  7. Mungu awalaze mahali pema peponi,amina
    na Mungu awape nguvu wafiwa katika kipindi hiki kigumu kwa kuondokewa na wapendwa wao.

    ReplyDelete
  8. Poleni wadau wote wa Limbachia na Royal Mushi kwa kumpoteza member.

    ReplyDelete
  9. Pole mzee wetu Mwapachu na familia kwa msiba huu wa Harith. Tulikuwa naye The Grange school Nairobi Kenya kwa niaba ya wale wote waliosoma naye Nairobi Tunasema Mungu alitoa, mungu ametwaa ailaze roho ya marehemu Harith pahala pema peponi AMEN

    ReplyDelete
  10. yes that is Harith mdogo wake Hamza aliyekua Arusha School

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...