![]() |
Dkt Harrison Mwakyembe akiwa na Mh Victor Mwambalaswa Bungeni Dodoma siku zilizopita |
Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe leo amepelekwa nchini India kwa matibabu zaidi ya ugonjwa wa ajabu uliomuanza kiasi cha miezi mitatu iliyopita kabla ya hali kubadilika siku za karibuni na hatimaye mwili wake kunza kuvimba na ngozi kuharibika.
Msemaji wa familia ambaye pia ni Mbunge wa Lupa Mh Victor Mwambalaswa amesema kwamba hali ya ngozi Dk Mwakyembe ni mbaya, japokuwa ana nguvu zake na fahamu na anaongea bila shida na anatembea mwenyewe.
Viongozi kadhaa akiwemo Waziri wa Ujenzi Dk John Pombe Magufuli walikuwepo Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar kumsindikiza Dk Mwakyembe, ambaye jana alitembelewa na Rais Jakaya Kikwete nyumbani kwake Mbezi Beach.
Kwa mujibu wa mke wa Dk Mwakyembe, Mama Linah Mwakyembe, daktari wa mumewe amesema mgonjwa anasumbuliwa na ugonjwa wa ngozi unaojulikana kitaalamu kama Exfoliative Dermatitis.
“Alianza kuugua muda mrefu kidogo, kama miezi mitatu iliyopita, hali hiyo ilikuwa inatokea na kupotea hadi sasa ambapo hali imekuwa mbaya zaidi,” alisema.
Alisema madaktari waliomfanyia uchunguzi kwa nyakati tofauti katika kipindi hicho walitoa majibu tofauti na kuongeza kuwa wapo waliosema hali hiyo ilisababishwa na kisukari na mwingine ambaye hakutaka kutaja jina lake, alisema kulikuwa na chembechembe za sumu katika damu yake.
“Baada ya ngozi yake kubadilika sana na hali kuwa mbaya, tulienda hospitali na madaktari walitupa majibu tofauti, wapo waliosema ni kisukari na kuna mwingine alisema kuna chembechembe za sumu,” alisema Linah na kufafanua kuwa daktari aliyedai hivyo hakuwapa maelezo zaidi.
Alisema madaktari waliomfanyia uchunguzi kwa nyakati tofauti katika kipindi hicho walitoa majibu tofauti na kuongeza kuwa wapo waliosema hali hiyo ilisababishwa na kisukari na mwingine ambaye hakutaka kutaja jina lake, alisema kulikuwa na chembechembe za sumu katika damu yake.
“Baada ya ngozi yake kubadilika sana na hali kuwa mbaya, tulienda hospitali na madaktari walitupa majibu tofauti, wapo waliosema ni kisukari na kuna mwingine alisema kuna chembechembe za sumu,” alisema Linah na kufafanua kuwa daktari aliyedai hivyo hakuwapa maelezo zaidi.
Kwa mujibu wa Linah, ngozi ya Dk Mwakyembe inawasha na inakuwa kama inatoa mba mwili mzima hadi kichwani.
Pole sana kiongozi wetu shupavu. Watanzania wenye uchungu na nchi yetu na rasilimali zilizomo tunakuombea kila la heri, upone haraka na urejee nyumbani kutusaidia kimaendeleo. Mungu akusaidie upone haraka mkuu. Tunakupenda sana.
ReplyDeletepole dokta,kwanini india? Napatwa na mashaka na madaktari wetu,hayo ni majibu mawili tofauti kutoka kwa mabingwa wa afya zetu.huyo ni mtu mkubwa anapewa majibu kama hayo je mimi mzaramo toka chole itakuwaje.majibu yenyewe yanajionyesha kipimo kilikuwa ni macho,wa tz tumekwisha.
ReplyDeletePole mheshimiwa, hiyo ni kadar ya Mwenyezi Mungu
ReplyDeletePole sana mwanaharakati wetu wa ukweli,nakuombea kwa mungu inshallah utapona.Tupo pamoja Dr!!
ReplyDeleteDr. Mwakyembe, nakushauri wewe na mkeo mwende Synagogue Church of All Nations (SCOAN), Lagos- Nigeria kwa Prophet TB Joshua UKAOMBEWE. Bwana YESU atakuponya.
ReplyDelete