Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda leo akichangia wakati wa mjadala kuhusu fedha na mdororo wa uchumi duniani ambapo amezitaka nchi zilizoendelea kutojisahau kwa kudhani kuwa maendeleo ya nchi hizo hayana uhusiano wa moja kwa moja na nchi zinazoendelea. Hivyo mataifa yote yanahitaji kuungana na kufanyakazi pamoja. Kulia kwake ni Kamishna wa Bunge Mhe. Hamadi Rashid Hamadi ambaye alihudhuria kikao hicho.
Makamu wa Rais wa Kamati ya Bunge la Dunia inayoshughulikia maendeleo endelevu, Fedha na Biashara Mhe. Hamad Rashid Hamad ametaka Umoja wa Mataifa kusikiliza kilio cha muda mrefu cha mataifa machanga cha kupata uwaklishi ulio sawa katika vyombo vya kutoa maamuzi hasa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, vyombo vya fedha (IFM,WB) na kuongeza uwazi katika chombo cha kimataifa cha Biashara (WTO) ambacho kwa muda mrefu kimekuwa kikiwatajirisha matajiri na kuwaumiza wazalishaji wan chi maskini. Mhe Hamadi (kati) akiwa na Mhe. Susan Lyimo na Mhe. Angela Kairuki amesema kinachotakiwa ni mgawanyo wa madaraka na siyo wa utajiri tu.
Mhe. Suzan Lyimo na Mhe. Angela Kairuki wakifuatilia majadiliano ya wajibu wa wabunge wa kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora ya afya kwa wanawake na watoto ambapo ujumbe wa Tanzania ulielezea mafanikio yaliyofikiwa katika kutekeleza malengo namba nne na tano ya millennia ikiwa ni pamoja na changamoto zake.
Kaimu Katibu wa Bunge Bw. John Joel akishauriana na Katibu wa msafara Bw. James Warburg kwenye kikao cha Chama cha Makatibu wa mabunge wa IPU kabla ya uchuguzi wa Rais wa Chama hicho leo.
Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Abdulrahmin Abdi akihutubia Baraza Kuu la IPU na kuitaka dunia iisadie Somalia badala ya kuishia Afrika Mashariki peke yake.
Viongozi mbalimbali wakiifuatilia hotuba ya Mhe. Abdi kwa makini
Spika Makinda na Mhe. Hamadi wakibadilishana mawazo na mjumbe wa IPU
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Masha Fortunatus afuatilia mjadala.
Uganda ndiyo itakayoandaa mkutando wa IPU Marchi 2012. Haya ni baadhi tu ya maandalizi ambao wameanza kufanya kwa ajili ya mkutano huo. Vyombo vya muziki wa utamaduni.Picha zote na Prosper Minja-Bunge
Tunafurahi viongozi wa bungeni wakikaa kwa pamoja kama hivi kujadili maendeleo bila kujali chama,namuona mheshimiwa hamad anashiriki vizuri hapo. Sio kama wale wenzetu wa kutoka nje ya bunge na kuzunguka mikoani kufitinisha na kupotezea wananchi muda wa kuzalisha wakati uchaguzi ulikwisha.
ReplyDeleteNapa ni utalii tu. Mbona hatuambiwi tija kwa taifa iko wapi?
ReplyDeleteNdugu yangu waliojumuika hapo ni wabunge wa mabunge yote toka kila nchi wakiwa wamewatuma wawakilishi wao,unaposema kuwa Mh Hamad yupo hapo si kuwakilisha chama bali nchi husika,hivyo una uhuru wa kutoa maoni,lkn uangalie kichwa cha habari husika.Bado tuna kazi endelevu kufikia ukomavu kisiasa kumbuka.
ReplyDelete