Wapiganaji toka vyombo mbalimbali vya habari wakisubiri nje ya ukumbi wa White House wa makao makuu ya CCM mjini Dodoma leo

Baadhi ya wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM wakisubiri 
kuanza kwa kikao cha leo.
 Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo katika siku ya kwanza ya kikao chake cha siku mbili kinachoendelea mjini Dodoma imefanya uteuzi wa makatibu 10 wa CCM wa wilaya .
Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye  walioteuliwa kuwa ni Makatibu wa wilaya wapya walioteuliwa ni kama ifuatavyo: -
1. Ndg. Zainabu Mlawa,
2. Ndg. Paulo Mwita,
3. Ndg. Magdalena Ndwete,
4. Ndg. Ramadhani Sevingi,
5. Ndg. Odilia Maholelo,
6. Ndg. Omari Zuberi Mbwana
7. Ndg. Raymond Mangwala,
8. Ndg. Yahya Saleh Issa,
9. Ndg. Ame Omar Mkadam
10. Ndg. Langael Akyoo
Pia Kamati Kuu ya CCM imetengua uteuzi wa Makatibu watatu wa wilaya na kuwapangia kazi nyingine. Makatibu hao ni:-
1. Ndg. Zubeda Mbarouk aliyekuwa Kwimba
2. Ndg. Mussa Wenema aliyekuwa Kilindi
3. Ndg. Mkongea Ally Pira aliyekuwa Wilaya ya Magharibi.
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa inafanyika tarehe 21 na 22/11/2011 na kufuatiwa na kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kitakachofanyika tarehe 23 na 24/11/2011. Kikao hicho na vingine vinafanyika chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Baada ya kumalizika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa tarehe 25 hadi 27/11/2011 kutafanyika Semina ya Watendaji wa Chama Cha Mapinduzi wa ngazi ya Kitaifa hadi Wilaya. Katika semina hiyo watakaoshiriki ni Wajumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa, Sekretarieti za Jumuiya za Chama Cha Mapinduzi (UWT, UVCCM na WAZAZI), Makatibu wa CCM wa Mikoa na Wilaya zote nchini.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. ndugu ndugu imetokea wapi tena. mimi nina jamaa yangu hapo na hapendi kuitwa ndugu so and so. hayo yaliisha bwana.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...