Wananchi wakiwa wamekusanyika katika Banda la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu kutaka kujipatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyokuwa ikitolewa kwenye Banda hilo,wakati wa Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru ya Wizara wa Katiba na Sheria katika viwanja vya Mnazi Mmoja,jijini Dar es Salaam.
Ofisa wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali akihangaika jinsi ya kugawa Katiba kwa watu waliofurika katika banda la ofisi hiyo.
Wananchi wakihangaika kupatiwa Katiba.
Ofisa Sheria kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania,Mercy Mrutu akiwaeleza wanafunzi wa shule ya msingi Majukumu ya Tume wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
kila siku inasemwa katiba ya nchi lakini wananchi hawana katiba yenyewe.
ReplyDeleteama kweli tunahitaji watu wa kulikomboa taifa hili...kwa nin siku zote katiba haikugawiwa kwa wananchi kama njugu kama wanavyogawa sasa..kwa kuwa wameona kuna dalili za kuisha muda wake au vipi?...tanzania!, kazi tunayo.ni haki ya kila raia kuijua katiba sasa kwa nn siku zote hawakuwagawia wananchi?...ukitaka kuipata ni ngumu kupatikana na mara unapata iliyofeki na si halisi hasa kwa wale waliokuwa wanaitafuta kwenye mtandao kama mimi.inasikitisha sana bwana mwanasheria mkuu kwa kweli...mimi sina chama lakini huwa wakati mwingine nawaona chadema kama wanataka kuttuletea vurugu lakn upande mwingne hawa ccm ndo onyoo kabisaa sasa mtu unashindwa uelekee wapi unaamua kufa kiume tu...
ReplyDelete