Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Mhe. Ombeni Sefue (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wabunge wa Tanzania ambao ni viongozi wa Chama cha Wabunge wa Jumuiya ya Madola (CPA) tawi la Tanzania walipomtembelea Ofisini kwake New York, Marekani wakiwa njiani kuelekea Dominica, West Indies kwa ziara ya mafunzo, pichani kutoka kushoto ni Mhe. John Paul Shibuda, Mb wa Maswa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya CPA Tanzania, Mhe. Mussa Azzan Zungu,Mbunge wa Ilala na Mwenyekiti wa CPA Tawi la Tanzania, Mhe. Lucy Owenya, Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya CPA ya Tanzania na Nd. Saidi Yakubu, Katibu wa Msafara huo na Afisa Mratibu wa Masuala ya Jumuiya ya Madola Bungeni
Balozi Ombeni Sefue katika mazungumzo na Waheshimiwa Wabunge Ofisini kwake.
Wabunge wa Tanzania wakitembelea jengo la Ubalozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa lililonunuliwa hivi karibuni ambapo Ubalozi huo unatarajia kuhamia, wa pili kulia ni Mama Rose Mkapa, Afisa Utawala wa Ubalozi huo.
Mama Rose Mkapa akitoa maelezo kwa wabunge wanaomsikiliza kwa makini walipotembelea moja ya ofisi zilizoko katika jengo hilo lenye ghorofa sita ambalo Ofisi ya Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa inatarajia kuhamia na pia kutoa fursa kwa wapangaji wengine kupangisha ndani ya jengo hilo.Wabunge hao walitembelea jengo hilo kujionea wenyewe ikiwa pia ni sehemu ya kazi zao kama wawakilishi wa wananchi hususan Mhe. Mussa Azzan Zungu, Mb na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na Mhe. John Paul Shibuda,Mb ambae ni Mjumbe wa Kamati hiyo.Picha kwa hisani ya Ofisi ya Bunge.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. pesa yetu ya kodi ndio inavotumika hivi,! hospitali muhimbili wagonjwa wanalala chini na dawa hakuna, temeke wanajifungulia chini kwenye sakafu ! serikali haina pesa , wabunge wanavinjari kila kukicha ! tutafika kweli Tanzania?

    ReplyDelete
  2. Annony wa 23, 03;14 PM. Mbona wapigia mbuzi gitaa na si mpiga kura? Kapige kura!

    ReplyDelete
  3. huyu rose mkapa ndio mkewe yule aliekuwa rais mkapa?

    ReplyDelete
  4. sasa hawa mabalozi wenu wakakae wapi. Kupanga nyumba huku majuu ni ghali mno. Lipi bora, wewe unaelalamika umejitolea nini katika maisha yako katika kujenga nchi yako. Tangu utoke kijijini kwenu umesharudi kuona nini unaweza kusaidia. Ni mimi na wewe na yule anaetakiwa nchi hii.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...