Umoja wa watanzania waishio ubelgiji (Watanzania Belgium) kwa kushirikiana na ubalozi wa Tanzania nchini ubelgiji pamoja na marafiki wa watanzania waliopo ubelgiji wanayofuraha kuwatangazia watanzania wote pamoja na marafiki wa watanzania kuwa kutakuwa na sherehe ya kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika/Tanzania Bara siku ya tarehe 10/12/2011. Sherehe hizo zitafanyika katika ofisi za ubalozi wa Tanzania Ubelgiji kwenye anwani ifuatayo:
72 Ave.Franklin Roosevelt
1050 Brussel
BELGIUM.
Kwa wale wenye nafasi na uwezo wa kufika tafadhali thibitisha ushiriki wako kwa kuandika barua pepe kwenye anwani:dmwasha@gmail.com
Nyote mnakaribishwa
MIAKA 50 YA UHURU:::::::::::::::::;
ReplyDeletePongezi Watanzania mnaoishi Ubelgiji kwa shamra shamra hizi za Uhuru wetu!
Iisipokuwa, inasikitisha kuwa ikitokea na mimi nije kuungana nanyi kwa sherehe hizi nitakwama Ubalozini kutokana na Urasimu wa MTUMISHI MMOJA WA KIKE WA KIHINDI ANAEPOKEA MAOMBI YA VIZA HAPA UBALOZINI DAR ES SALAAM.
HUYU MAMA NI VERY CORRUPT NA ANAFANYA KAZI KWA KUWABANIA WAKONONGO NA KUTOA UWEZEKANO WA VISA KWA WAASIA NA WAHINDI TU!
HEBU FANYENI MPANGO MFIKISHE KADHIA HII HUKO KTK VYOMBO VYAO VYA SERIKALI YA UBELGIJI AMA SIVYO TUTASHINDWA KUWATEMBELEA HUKO!