
Kama nilivyoelezea mara kadhaa katika blogu zangu, tulizunguka sehemu mbali mbali, kama vileKalenga, Matema Beach, Lyulilo naBagamoyo. Baada ya mizunguko hiyo niliwafikisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, nami nikarejea Marekani kwani muhula wa masomo ulikuwa unaanza.
HABARI KAMILI BOFYA HAPA
Hehe Profesa wasomesha wazungu!!
ReplyDeleteKwa maProf.km huyu mbona kazi ipo nikujikweza kwakwenda mbele..hahahah
ReplyDeleteMdau anonymous, shukrani kwa ujumbe wako. Nilianza kufundisha mwaka 1976, hapa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mwaka 1991, kutokana na sababu mbali mbali, nilifika kwenye chuo nilipo huku Marekani, kufundisha katika idara ya ki-Ingereza.
ReplyDeleteNataka vijana wetu wa Tanzania wasikie hivyo, ili wajijengee moyo wa kuzingatia masomo kwa dhati kama nilivyofanya tangu nilipokuwa kijana mdogo. Kwa kufanya hivyo, nao wataweza kufika mbali. Wasome na kujielimisha kwa bidii sana na kwa dhamiri moja. Hakuna njia za mkato katika masuala haya.
U dont get it, kazi kweli.
ReplyDeleteNa wewe anonymous wa pili hapo juu, una matatizo. Kazi niliyosomea na ninayofanya ni ualimu, si uchawi.
ReplyDeleteNi wajibu wa mwalimu kuelezea yale anayoyafahamu, anayotafiti na anayofanya katika taaluma na mengine yahusikayo.
Kwa profesa, wajibu huo ni pamoja na kuandika makala na vitabu, ambavyo vinachangia taaluma, na papo hapo vinamtangaza yeye.
Hiyo mipango ya ushirikiano baina ya vyuo, ambayo nimeielezea nayo ni suala la kuelezwa mbele ya walimwengu. Kutokana na kuelezea huko watu makini wanaotaka kuanzisha programu za aina hiyo, wakiwemo wa-Tanzania, wananitafuta ili niwape ushauri. Vile vile wanafunzi wanaotafuta program za kujiunga nazo wanatafuta ushauri wangu.
Kutokana na kuandika vitabu na makala, ambayo nayo ni namna ya kutangaza taaluma na kujitangaza mimi mwenyewe kama mwanataaluma, wengi, wakiwemo wa-Tanzania, wananitafuta ili niwape miongozo na ushauri. Nami sijawahi kuwapuuzia, bali nafanya kila niwezalo kuwamegea ninachojua.
Hao ni watu makini, tofauti na wewe ambaye akili zako zimelala. Una mawazo ya wachawi, ambao wanajificha wasijulikane. Kauli yako imenikumbusha kitu kimoja. Nimepita sehemu kadhaa za Tanzania ambako watu wanaogopa hata kujenga nyumba bora, kwa sababu wataonekana wanajikweza, na sehemu zingine wanakuambia kabisa wanaogopa kulogwa. Naona huu ndio utaratibu unaoutaka wewe, ila usitegemee kama nitayumbishwa na watu kama wewe.
Prof. Mbele, Hongera kwa kazi yako,Pole kwa kueleweka vibaya kwa baadhi ya watu na pia endelea na kazi yako.
ReplyDeleteBaadhi ya watu sio waelewa kwa vile wanachukulia Social media kama hii blogu ni sehemu ya kujikwezea kumbe sio hivyo.
Kwa maelezo yako ya maoni ya tano 5 hapo juu yamejitosheleza kwa sababu kazi yako ni Muhadhiri na muelimishaji na kuwa unahitaji kuwafikia wengi kadri iwezekanavyo ili mawazo yako yafike na pia uweze kubadilishana mawazo na wengine.
Mfano ktk blogu hii ili kuthibitisha hilo tumeona baadhi ya watoa Maoni wakiendesha Experiments (Majarobio ya kisayansi ) na kuwezesha mawazo yao kuwafikia wengi huku ikiwa ni maoni yao tu kulingana na mtazamo wao!.
Hii blogu ni sahihi kama ulivyofanya Prof. Mbele kutumika kama njia ya kuelemishana ,kutoa kile ulicho nacho mfano elimu na shughuli zako ili tushirikiane kwa faida ya wote!
Mdau mtoa maoni wa pili, tafadhali elewa kuwa kwa mtu al;iefikia kitwa 'Prof. Mbele' huku akiwa anafundisha ktk nchi za wanaofahamu kama Marekani tayari amekwisha kuwa maarufu hivyo hana anachotafuta ktk blogu hii zaidi ya kuifikisha fikra zake na kazi ya mikono yake na kushirikiana na wengi kwa nia ya wote kunufaika!.
ReplyDeleteDunia imekuwa kijiji kwa uwepo wa teknolojia za kisasa za mawasiliano.
Hakuna njia ya muujiza kwa watu kufikiana isipokuwa vitu kama hii blogu ''social media'' huku Ankali akituwezesha!
Mdau mfano wa matumizi mazuri na endelevu ya ''social media'' kama anavyofanya Mdau Prof.Mbele kuwafikia wanafunzi wake kielimu kwa njia ya blogu, ni zile experiments (majaribio ya kisayansi) zilizofanywa ktk maoni ya wadau kama ile posting ya UZURI WA TAUSI DUME, inafurahisha watu wakilumbana kwa hoja na mifano hai kupitia Blogu ya jamii!!
ReplyDeleteBlogu ya jamii ifahamike kuwa sio ''exposure'' bali ni uwezeshwaji wa watu waliokuwa sehemu tofauti kijiografia kuwa pamoja kifikra!
Profu. Acha kubishana na hawa watoto wa tandamti.
ReplyDelete