Msanii wa Muziki wa Dansi nchini,Charles Gabriel a.k.a Charles Baba akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo wakati akizungumzia nia yake wa kujitoa rasmi katika Bendi yake ya awali ya African Stars (Twanga Pepeta) kwenye mgahawa wa Hadee's uliopo katikati ya Jiji.Charles Baba  pamoja na kutangaza nia yake hiyo,pia amemtangaza Meneja wake Mpya,Bw. Bernard Msekwa ambaye atasimamia shughuli zake zote za Kimuziki ikiwa ni pamoja na kuingia mikatana na Bendi yeyote itakayomuhitaji.
 Meneja Mpya wa Msanii wa Muziki wa Dansi nchini,Charles Baba ,Bw. Bernard Msekwa akisisitiza Jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na msanii wake huyo leo kwenye mgahawa wa Hadd's uliopo katikati ya jiji la Dar es Salaam leo.
Baadhi ya Waandishi wa habari waliofika kumsikiliza Msanii huyo pamoja na Meneja wake wakisikiliza kwa makini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Yaani bongo ukitaka upaishwe hewani kwa ghafla, tafuta msanii yoyote na utangaze wewe ni meneja wake.. Tambararee..!!

    ReplyDelete
  2. Charles Gabriel aka Baba ni mwanamuziki mzuri sana hadhi ya kina Choki na anastahili kuwa na bendi yake mwenyewe. Kaza buti dogo onyesha kipaji chako we will support you ila usipige fleva itakulostisha. Kama utaweza mchukue Barnaba kwenye bendi yako, yule dogo anaimba ila anaharibu sauti yake kuimba nyimbo ama muziki usioendana na sauti yake. Shughulikia hili suala.

    ReplyDelete
  3. Charles utajuta kilicho kutoa Twanga huyo sio!!!

    ReplyDelete
  4. Sijui Twanga Pepeta kuna nini, mtu akiondo huwa anarudigi mwenyewe tu..kuna wakati choki aliondoka akarudi hata sasa hasikiki, Kocha wa dunia naye alihangaikaa baadae karudi.

    ReplyDelete
  5. TWANGA!!!!! KUNANI KULEEEE!!!MBONA KILA MSANII ANATIMKA!!!!!!!

    ReplyDelete
  6. Umejimaliza mwenyewe, unatoka Twanga!!!Waulize wenzio mapacha watatu wako wapi sasa?

    ReplyDelete
  7. aende huko hana lolote, meneja bongo!

    ReplyDelete
  8. Charles hongera kwa uamuzi wako,usitishwe na mashabiki uchwara,ukiwa mwoga ktk kutafuta maisha utakufa maskini,Ona wenzio akina Chokky,Mapacha watatu nk.wanaenedelea vizuri,wewe haukuzaliwa Twanga,pia kwa wasanii wengine inabidi mtafute mabadiliko na maendeleo ya maisha yenu na siyo sifa,Big up Charles.

    ReplyDelete
  9. Chaz umetisha ila huyo manager chaka ni mzee wa mjini ila big up kaka

    ReplyDelete
  10. nenda kaongee na rafiki zako kina jose mara na chokoraa, na kalala kama mlivyopanga hapo awali iwe mapacha original mtatishaaaa balaaa!!! NI wakati wa kuondoatofauti na kufanya kazi na kuleta burudani holla..!!

    ReplyDelete
  11. Hongera dogo ni maamuzi mazuri, katika kila penye maendeleo watu walithubutu ndio wakafanikiwa, naamini wewe umeamua kuthubutu basi utafanikiwa usiziogope changamoto zozote wadau na washabiki wanazokupa ww zichukulie hizo zote ni changamoto kwako za maendeleo yako. KAPINGAZ Blog.

    ReplyDelete
  12. Twanga inaonekana ni Chuo cha kuwatengeneza wanamuziki mpaka wakaweza kuwika na kuuzika. Huyu Chalz Baba inasemekana kajiunga na Bendi ya Mashujaa inayomilikiwa na Sakina Trans na mumewe Maisha ambao ni marafiki wa karibu wa Asha Baraka kwa kitita cha Shs milioni 15 na marupurupu mengine. Sasa hapa sijui kama kutokana na mikataba ilivyo kama Twanga pepeta kama bendi wamelipwa chochote.

    ReplyDelete
  13. HUYO ANAENDA MASHUJAA BAND WANATUZUGA TU LAKINI POA HONGERENI MASHUJAA KWA KUONYESHA THAMANI YA WANAMUZIKI

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...