Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Injinia Stella Martin Manyanya (Mb) (wapili kushoto) na Wakuu wa Mikoa ya Tabora Mhe. Fatma Mwasa, Kigoma Kanali Mst. Issa Machibya (kulia) na Shinyanga Mhe. Ally Nassoro Rufunga wakiangalia moja ya mada zilizowasilishwa kwa njia ya projekta katika Mkutano wa Ujirani mwema Mikoa ya Kanda ya Magharibi mwa Tanzania uliofanyika Wilayani Nzega katika Mkoa wa Tabora. Mkutano huo ambao umefanyika leo umelenga kujadili mambo muhimu ya kimaendeleo na changamoto zinazoikabili Mikoa hiyo.
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Ijnjinia Stella Manyanya (kushoto) akimkabidhi zawadi ya kinyago maalum Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Fatma Mwassa. Kinyago hicho chenye picha ya watu wawili mume na mke wakiwa wamebeba kuni na kibuyu cha maji pamoja na shoka na jembe kama ishara ya pongezi kwa Mkoa wake kuandaa kikao hicho, Alisema kuwa "kuna usemi usemao mzigo mkubwa mbebeshe mnyamwezi", hiyo ni kutokana na kwamba wakazi wengi wa Mkoa wa Tabora ni Wanyamwezi hivyo akaona amkabidhi zawadi hiyo kama ishara ya Mkoa wake kukubali kubeba mzigo mkubwa wa kuandaa kikao hicho cha ujirani mwema.  
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Fatma Mwassa ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Mkutano huo akionyesha zawadi hiyo kwa wajumbe wa Mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...