NDUGU, JAMAA, WASHIRIKI NA MARAFIKI WOTE,

TAFADHALI FUNGUENI MIOYO YENU MPOKEE KHERI NA FANAKA KWA MWAKA MPYA 2012.

NAWASHUKURU NYOTE TULIOSHAURIANA NA KUFANYA KAZI PAMOJA HUSUSAN ZA KUJITOLEA KTK CHAMA NA JAMII MWAKA WOTE WA 2011. MUNGU AWAONGEZEE HEKIMA NA UJIRA WA MOYO WA UVUMILIVU.

JE MMESIKIA SIRI YA MWAKA (2012)=

-UKIWA NA WAZO LA KAZI UKALIBANIA MWENYEWE UJIRA WAKE =0
-KAZI UKIAMUA KUIFANYA MWENYEWE ITAKUGOMEA NAKUBAKIA =1
-KAZI HIYO UKIMSHIRIKISHA MWINGINE UTAPATA UJIRA WAKE =X2

HAYA MCHEZA SINDIMBA HUITIKA MDUNDO WA MPIGA NGOMA.

Maulana atupe TIBA na nafuu ya haraka na mauguzi yaliyotupata mwaka 2011, sisi na kaya zetu. Atuepushe na pepo mbaya za maradhi mwaka huu 2012.
Mwenye Enzi abariki kazi za mikono na jasho letu kwa mwaka wote 2012 na kuendelea.

KHERI YA MWAKA MPYA 2012.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Mdau wa UK hizo kelele zako zitakwisha April, ambako sheria mpya za UK zinaanza kutumika. Moja ya sheria mpya inahusu visa za highly skilled person ambayo inasema ili upewe viza inapidi uonesha umepata kazi ambayo mshahara wake sio chini ya £25,000/=.

    ReplyDelete
  2. wa anony wa 01;09
    we unachowaza ni visa tu...pole sana rafiki.
    Dunia itaendelea kukaliwa kila kona mpaka mwisho wa dahari.

    sasa salamu na maombezi ya kufunga/kufungua mwaka za huyu bwana/mama zina makosa gani? au mtimanyongo wako tu wa siku zote?

    Wabongo bwana tambarareeeee, lalama tu saa zote. Hata wanaodai haki hawazijui haki zao zilizopo na mpya watakazo.

    Al Karim

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...