Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya uchimbaji Makaa ya Mawe, Tancoal,Graeme Robertson, wakati alipotembelea mradi wa Uchimbaji Makaa ya Mawe unaoendelea eneo la Ruanda Wilaya ya Mbinga, wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Ruvuma jana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipiga picha ya kumbukumbu na Msanii Ofisa Utamaduni Mstaafu wa Wilaya ya mbinga, Benedict Maundi, baada ya kuzindua rasmi mitambo ya kuzalisha umeme na kuwahutubia wananchi wa Wilaya ya Mbinga akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Ruvuma, jana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akibonyeza kitufye ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi mashine za kuzzalisha umeme, wakati alipotembelea katika mradi huo uliopo Wilayani Mbinga akiwa katika ziara yake ya moa wa Ruvuma, jana. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Tanesco, Eng. Boniface Njombe.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akiweka Jiwe la Msingi katika mradi wa mashine za kuzalisha umeme Wilayani Mbinga, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Ruvuma jana.
Mkazi wa Mbinga ambaye ni mlemavu, akifurahia kwa staili yake wakati wa mapokezi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipowasili katika viwanja vya mradi wa mashine za kuzalisha umeme jana.
Mkazi wa Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuka akiwa na picha ya kuchora ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Mohammed Gharib Bilal, akipandda mti wa kumbukumbu baada ya kuzindua mashine za kuzalisha umeme Wilaya ya Mbinga, wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Ruvuma jana ambapo pia alitembelea na kukagua mradi wa uchimbaji wa makaa ya mawe ya Ruanda. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
hongereni tanesco
ReplyDelete