Mkutano huo ulitanguliwa na Mkutano wa Wataalamu uliofanyika tarehe 1 na kufuatiwa na Mkutano wa Makatibu Wakuu tarehe 2 na hatimaye leo Mawaziri. Mkutano ulijadili  maandalizi ya mkutano wa kilele wa umoja wa mataifa wa mazingira, katika ngazi ya Jumuiya. Waziri aliyeongoza Tanzania katika majadiliano hayo ni Mheshimiwa Fatma Abdulhabib Ferej, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar. Katika ngazi ya Makatibu Wakuu, aliyeongoza ni Ndugu Sazi Salula, Katibu Mkuu  katika ofisi ya Makamu wa Rais, wengine ni Ndugu Maimuna Kibenga Tarishi -katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii, Ndugu Uledi Mussa -naibu katibu mkuu wizara ya ushirikiano wa afrika mashariki na dkt Islam Salum, Naibu Katibu Mkuu wa Mazingira Zanzibar. Ngazi ya wataalam.iliongozwa na Dkt Abdullah Makame wa Wizara ya Afrika Mashariki akisaidiwa na Bertha Nyange Wa Wizara  ya Maliasili na Utalii. Wataalam mbali mbali walishirika kutoka sekta za umma na binafsi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. mitego hiyo ankarrr!! unaona enhe?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...