Na Mery Ayo,Arusha
MTOTO mdogo ajulikanae kwa jina la Tatu Ally mwenye umri wa miezi tisa mkazi wa sombetini katika halimashauri ya Arusha amefariki dunia baada ya nyumba aliyokuwa amelala kuteketea kwa moto.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa arusha Tobias Andengenye alisema kuwa tukio hilo limetokea mnamo february 18 majira ya saa moja na nusu usiku.
Alisema kuwa ajali hiyo ya moto iliunguza nyumba ya mtu aitwae Stephano Masawe (85)ambaye ni mstaafu wa mamlaka ya maji taka na safi (AUWSA )na hatimaye kuweza kusababisha kifo cha mtoto huyo.
Aidha kamanda alileza kuwachanzo cha moto huo kinasadikika kilitokana na mlipuko wa jiko lamafuta ambao ulienea kwenye chumba na hatimye kusababisha ajali hiyo.
Aliongeza kuwa moto huo ulianza kuwaka katika chumba cha mpangaji aitwae Neema Ally na ndipo baadhi ya mashuhuda walipiga kelele za kuomba msaada ambapo kwa bahati nzuri haukuweza kuenea kwenye vyumba vingine.
Aliongeza kuwa kujulikana kwa kifo cha mtotohuyo kulitokana mama huyo aitwae neema ally kueleza kuwa kabala ya ajali hiyo alikwenda dukani na kumwacha mtoto wake ndani na ndipo aliporudi alikuta moto umekwisha enea chumba kizima.
Mara baada ya tukio hilo walitoa taarifa katika kituo cha polisi ambapo askri waliokuwa doria katika maeno hayo walifika katika eneo hilo na kukuta mwili wa marehemu ukiwa kitandani mwa chumba hicho ambapo waliuchukua na kwenda kuuhifadhi katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mount meru
Kamanda alisema kuwa bado Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo.
Mnapokua mnatoa taarifa za huzuni na simanzi,jaribuni kuweka picha zenye kuendana na ujumbe husika.Nalisema hili kwa kusoma ujumbe wa kuungua kwa mtoto huyu halafu picha ya RPC akitabasamu.
ReplyDeletehakuna sababu ya kuweka picha ya kamanda wa polisi wa mkoa. Halafu anatabasamu.
ReplyDeleteSio tu anatabasamu, kaweka na posi haswaa!
ReplyDeletenawaunga mkono wadau hapo juu. Picha ya kamanda ya nini.
ReplyDeletenadhani bro michu yuko likizo hii isingetokea.
RIP mtoto, huyu mmwela shoga au vipi, unakenua nini wakatati mtoto kapoteza maisha wajameni!!
ReplyDelete