Mtoto Cesilia Edward (pichani) amefariki dunia jana saa tano usiku wa tarehe 08 katika hospitali ya Regency ya hapa jijini Dar es Salaam ambapo alikuwa amelazwa kwa siku mbili kwaajili ya matibabu
Marehemu Cesilia alikuwa na umri wa miaka 14 alikuwa na tatizo la moyo na figo kushindwa kufanya kazi na kusababisha tumbo kujaa maji na kuvimba.
aligundulika na tatizo hilo tangu alipozaliwa.
Kampuni ya Africa media Group wamiliki wa Channel ten Kupitia kipindi mimi na Tanzania ilifanikiwa kumpeleka mtoto Cesilia nchini India kwa matibabu mwaka 2011 mwezi Oktoba lakini hakufanikiwa kupata matibabu (operation) baada ya madaktari kuthibitisha kuwa alikuwa amechelewa kwa matibabu.
Cesilia alikuwa mtoto yatima na kulelewa na familia ya Bw. Peter Nyarugembe mkazi wa Mbagara kuu ambaye alikuwa akimlea baada ya kukuta akilelewa na dada yake wilayani Kisarawe na alimkuta na tatizo hilo ila kutokana na hali ya uchumi aliyo nayo hakuweza kumsaidia kupona ugonjwa alio nao na kuamua kuomba msaada kwa wasamalia wema kupitia Kipindi cha mimi na Tanzania.
Marehemu alifikishwa hospitali jumatatu ya tarehe 6 mwezi huu akiwa na hali mbaya iliopelekea kupoteza fahamu na kumbukumbu kila wakati hali iliendelea hivyo mpaka umauti ulipo mkuta.
Mungu ailaze roho ya marehemu Cesilia mahala pema peponi.
-Amen.



Pole sana mlezi pamoja na Dada wa Cesilia. Tunamuomba Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya Marehemu Cesilia, ipumzike kwa amani, Amen.
ReplyDeleteMwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amina
ReplyDeleteRIP - inauma lakini wanadamu tuna kikomo, tumwachie Mungu,
ReplyDeleteR.I.P CECILIA.
ReplyDeleteUNCLE NAOMBA, PICHA HII IBADILISHWE AU IONDOLEWE KABISA.
USHAURI WANGU.
Cecilia kapumzike kwa amani kwani umeteseka sana hapa duniani.
ReplyDeleteMungu akupe neema nyingi huko unakokwenda. Amin
Maskini, inauma sana, lakini yote ni mapenzi ya Mungu, inabidi tumshukuru. Ameteseka sana binti wa watu kwa kweli, Mungu ampumzishe katika amani yake sasa. RIP Cecilia.
ReplyDeleteWatanzania na wapendwa wote mliojitokeza kumsaidia binti huyu Mungu awalipe maradufu. Mzee uliyechukua jukumu la kumlea mtoto huyu na Dada Hoyce Temu, kazi yenu si bure mtalipwa na Mungu, mbarikiwe sana!
Mungu akuweke mahali pema na pumzika salama baada ya mateso ulikuwa ukiyapata mtoto Cecila Edward. Emin
ReplyDeletePoleni sana wafiwa ni kipindi kigumu kwenu na mungu atawaongoza na kuwapa nguvu kwa kipind hiki
ReplyDeleteR.I.P We will remember you always.
ReplyDeleteMungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.
ReplyDeletemungu akupe nguve Cecilia pumzika kwa amani,good night dear,kimeniuma sana nilipofungua hii blog kuona picha yako hoooooooooooooo yesu nalia mie,sikujui lakini wewe kama mtoto wangu.
ReplyDeleteCECILIA ULIPANGIWA NA MUUMBA WAKO MAISHA YAKO NA MUDA WAKO WA KUISHI HAPA DUNIANI, KWA HIYO SISI SOTE TUWAPITA NJIA HAPA DUNIANI, TUNAMSHUKURU MWENYEZI MUNGU KWA MAPENZI YAKE YOTE! BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LITUKUZWE MILELE YOTE AMINA!MUNGU BABA ULIYE KIMBILIO LETU NA ULIYEMUWEZA WA YOTE UMPE CECILIA PUMZIKO LA MILELE AMINA.
ReplyDeleteinna lilah waina ilah rajiun.
ReplyDeleteMLEZI WA HUYU MTOTO ANASUBIRI KUVIKWA TAJI MBINGUNI. NANI ANGEKUBALI MATATIZO YA KUUGUZA MTU ASIYEKUHUSU? MUNGU AKUTIE NGUVU.
ReplyDeletePUMZIKA KWA AMANI CECILIA
ReplyDeleteInna Lilah Waina Ilah Rajiun.
ReplyDeleteMungu awajaze nguvu na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu familia yote na ailaze roho ya Cecilia mahali pema peponi amen. So sad jamani
ReplyDeleteMungu ailaze roho ya Cecilia mahala pema peponi
ReplyDeleteInna lillahi waina ilaihi rajiuun, hana dhambi anaenda janna tu,
ReplyDelete