KIKOSI KAZI Ngoma Africa band aka FFU,
Wamevamiwa at facebook,msela moja amewamwagia mawe ya mapicha mabaya!

Kamanda Ras Makunja na rungu lake katika mshike mshike! 

Ughaibuni,
Leo na mapema bendi maarufu ya muziki wa dansi barani  Ngoma Africa band au maarufu kama FFU,
walivamiwa na maalamia katika kianzo cha kimoja cha www.facebook.com/ngomaafrica ambako msela
mmoja asiyejulikana alikichafua kianzo hiko kwa kumwaga picha za video chafu,kiasi cha kusababisha
usumbufu,fujo hizo za kutungikwa picha chafu katika kianzo cha FFU,zilishindwa kutulizwa na ngoma africa
wenyewe,kiasi kamanda wa bendi hiyo Ras Makunja akiwa ana ahaa na rungu mokononi ,lakini baadaye 
walipata msaada kutoka kwa mtalaam moja wa mambo ya IT ajulikanae kwa jina la Mfundo aka Boss,
kamanda Ras Makunja na mnyama wake mkali(pichani) alishindwa kuliziwia ghasia lililo ikumba bendi

Kumekuwa na baadhi ya wadau wenye uchokozi wanapoona kikosi hiko cha Ngoma Africa band aka
FFU kimetulia basi lazima watawatafutia shughuli ya kufanya! kwa kipindi hiki cha msimu wa baridi
kule ughaibuni kikosi kazi hiko kimejchimbia ndani ya kambi na kupiga kwata juu ya barafu.

Wakati Ngoma Africa band wanachua chua maumivu ya pilika pilika za kuvamiwa,wadau
tusikose kujipa burudani kamili bofya at www.ngoma-africa.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. kamanda mkuu wa ffu pole sana na mkasa huu,lakini sio kila fujo unaweza kuituliza kwa virungu,poleni sana sana
    Ndio ukubwa

    ReplyDelete
  2. kibaka amepenyaje? katika kambi ya ffu,kama si uzembe wa askari waliokua lindoni,kamanda fukuza kazi
    askari hao.

    ReplyDelete
  3. Yale yale,

    HUO NDIO ULE WIVU USIOENDELEVU:

    Huyo aliye chafua ukurasa katika facebook ya Ngoma Afika Band sio mwingine ila ni mwenye wivu usio endelevu tuliokuwa tunaujadili humu wiki iliyopita.

    Ngoma Afrika Band wamepigana na wakafika hapo walipo, kwa hivyo wanaotaka kufikia ngazi hiyo wafanye Ushindani kwa njia zinazokubalika na sio NJIA ZA WIVU HASI!

    ReplyDelete
  4. Jamani kiswahili chako vipi wewe kikosi kazi Hiko ni kiswahili gani?
    Tujitahidi sisi Watanzania kuandika Kiswahili sanifu jamani.

    ReplyDelete
  5. Fitina, Majungu na Wivu havina Chuo wala Mtaji!,

    Masikini weee akina Ras Makunja wa wenzake Ngoma Afrika Band wanawangiwa mchana kweupe kwa njia ya mtandao na tekinoloji ya kisasa,

    Mmeona Wanga wasivyo na hala wala kujua vibaya?

    ReplyDelete
  6. NGOMA AFRICA BAND AKA FFU KAZENI BUTI

    Ngoma Africa band ni wapiganaji wa kweli katika gemu la burudani ya muziki,pia wanapaswa kuungwa mkono,kwa mafanikio ya kufukia kiwango walichofikia,lakini hapa inaonekana kuna kuna baadhi ya wauni
    wanajaribu kuwachafulia,baadala ya kuwaunga mkono.

    ReplyDelete
  7. mkuu kikamanda ketu ras makunja,mnaletewa vituko mchana mchana,kweli wabongo tuna safari ndefu,wenzetu wanatumia social media kujitangaza duniani lakini sisi bado tunafikira finyu

    ReplyDelete
  8. I have a feeling hawa watakuwa Clouds media, wasanii wa fleva ama wapenzi wao ndiyo wanafanya hivi ili wakuze muziki wa big g (fleva), kumbukeni watu wa Clouds media kuwa original ni original tu hata mfanye nini hamuwezi kupiku, ila big g utamung'unya kisha utamu unaisha na mchezo kwishney! Poleni sana mabalozi wetu kazeni buti na endeleeni kupeperusha bendera yetu huko anga za juu, achaneni na hao Clouds media minded people.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...