Akikabidhi msaada huo wa madawati meneja wa Benki ya NMB kanda ya nyanda za juu kusini Bi.Lukesia Bena amesema benki yake imetoa msaada huo baada ya kuridhia ombi lililotolewa na mbunge wa jimbo la Mbeya mjini Joseph Mbilinyi kwa benki hiyo kusaidia madawati kwa shule za msingi ili kuwajengea uwezo wanafunzi kupenda masomo
Benki ya NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imetoa msaada wa madawati mia moja na kumi kwa shule za msingi Sinde, Maanga, Lyoto na Ilomba ili kuboresha huduma za elimu kwa shule hizo.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya mkurugenzi wa jiji la Mbeya Afisa elimu wa shule za msingi jiji Bi.Aurelia Luensi ametoa shukrani kwa uongozi wa Benki hiyo kuchangia katika elimu na kuwasihi walimu na wanafunzi kuyatunza madawati hayo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...