WANAFUNZI WA TANZANIA MISRI ( T.S.U) pamoja na watendaji wa Ubalozi nchini Misri. Jumuiya na umoja wa watanzania kwa niaba ya wanachama wao walimkaribisha kwa hutuba fupi kisha Mh. balozi aliwapa watanzania hao nasaha jinsi wanavotakiwa wawe hapa ughaibuni kua na ushirikiano wadhati baina yao na kufanya malengo waliyoyakusudia lakini yawe yakihalali nakutshiri katika mambo yasiotendea haki nchi yao, pia kutosahau walikotoka waegemeze fikra zao nyumbani kwa kua taifa na familia ziinawategemea wao.
Pichani waliokaa kutoka kulia ni Mr.Jestas A. Nyamanga Minister Counsellor and Head of Chancery,Muheshimiwa Balozi Mohamed Haji Hamza na Bw Idrissa Kheir Juma Minister Counsellor. Waliosimama nyuma kutoka kushoto Bw. Abdallah Daruweshi Said mfanyakazi wa Ubalozi na Mweka hazina katika Jumuiya ya watanzania (TSE) wapili nyuma Bw. Seif Suleiman Kibwana Katibu Mkuu Jumuiya ya Watanzania Misri (TSE) Watatu Bw. Saidi Katibu Mkuu wa wanafunzi (TSU) wa mwisho Bw. Fadhili Mansour Mwenyekiti wa wanafunzi (TSU) ama picha zingine ni zapamoja Muheshimiwa na viongozi wengine wa Watanzania. Chini ni Mh balozi na wadau wengine wa TSU na ubalozini hapo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...