Na Deogratius Kilawe
Dunia sasa ni kijiji hamna namna ya kufanya kuepuka,ni uwanja wa kukabiliana na yote hayo mazuri na mabaya,Nimekutana na mikasa mingi hapa kwetu afrika watu wengi wakitumia intaneti pasipo faida ya kiuchumi au kijamii na kuwaletea majanga ya kupoteza rasilimali muda  pasipo sababu rasmi.

Mara kadhaa imenitokea wakati nikiwa miaka ya mwishoni mwa 1990’s  na mwazoi mwa mwaka 2000’s wakati ndio nilikuwa nipo sekondari nikiingia intaneti café pasipo sababu maalumu,mara  nimefungua tovuti hii,ile na kwa kuwa sikuwa najua tovuti mbalimbali  nikabaki najua google,yahoo,na baadhi tu,lakini kumbe kulikuwa na tovuti muhimu sana ambazo nilikuwa nakosa kupata taarifa nilizokuwa nazihitaji.

Nimeamua kwa moyo mkunjufu kushirikiana na umma  kujua  hili jambo,naamini sio wote lakini ni wengi huingia mitandaoni pasipo au hutaka kupata taarifa lakini kwa sababu ya kukosa taarifa ya tovuti gani nzuri na hivyo kuishia kukosa taarifa muhimu.
UKITAKA MAMBO YA BIASHARA:
MIKUTANO NA USAHILI/INTERVIEW YA ONLINE:
TAARIFA YA HABARI ZA TANZANIA, AFRIKA NA DUNIA
MASWALA YA KIROHO ,HALI YA HEWA , UBINADAMU PAMOJA NA KUJITOLEA
HABARI ZA BURUDANI  DUNIANI NA TANZANIA

KUJUA HABARI ,TAFITI ZA MAMBO NA VITU(MAKTABA YA DUNIA)
PICHA ZA KITAALAMU  NA KUNUNUA PICHA:
MITANDAO YA KIJAMII:
KUNUNUA VITU  MFANO VITABU NK.
MASWALA YA NDOA
Pangilia unachotaka kufanya kwa intaneti,usifanye tu kwa sababu linatokea,kifalsafa tunasema usipopanga  jambo,sio kwamba hujapanga,ila umepanga lolote ambalo litakalo kukuta na likuchuke.Hivyo matumizi ya intanet angalia sana yasiibe sana rasilimali muda yako.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. umeanza vizuri ukaendelea kipuuzi.

    ReplyDelete
  2. sawa tumekusoma ,usihukumu kama unatoa ushauri wa kutumia internet,stick to the point! Asanye lakini kwa kutusaidia japo umetuhukumu!

    ReplyDelete
  3. aslaaama alekum/ shalom
    napenda kutoa maoni kuwa huyu bwana amefanya vizuri sana sana na naomba watu waliojaliwa moyo huu wajitokeze zaidi. kwa mtazamo wangu sikuona kitu chochote kibaya bali amesema ukweli kwa wale wanaoadhirika. the truth hurts poleni. well done and keep it on.

    ReplyDelete
  4. Mdau tunakushukuru kwa kutuongezea elimu kidogo, Mungua akubariki uendelee kutujuza zaidi. Kwa wale wanaolaumu na kujiona wanajua zaidi, basi waonyeshe na kuthibitisha ujuaji wao kwa kuchangia na kuongeza points zaidi katika mada iliyowasilishwa badala ya kulala tu

    ReplyDelete
  5. ahsante bwana mkubwa ulimwengu unatakiwa uwe na watu wa aina yako tuweze kusogea mbele. Nami naongezea.

    kwa wale wapenzi wa music tv http://www.tmtv.co.tz/

    wapenzi wa zilipendwa za kongo

    http://soukous.com/

    for the geographers

    http://www.gomapper.com/

    Kazi kwenu,

    ReplyDelete
  6. asante saaana nilikuwa nahitaji sana hii mambo, na wale wenye roho za kwa nini mtajiju, mnabana hadi link mfaidi wenyewe, inahuu?

    ReplyDelete
  7. Ahsante Mdau Deogratius Kilawe.

    Kwa Uamsho wako kwetu juu ya matumizi endelevu ya Mtandao!

    Nilikuwa nafahamu masuala kadha wa kadha lakini hii taarifa yako imenifunua zaidi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...