Mama anayejishughulisha na kuuza samaki pembezoni mwa lango kuu la kuingilia katika soko kuu la manispaa ya Songea (kushoto) akimfungia mteja wake kitoweo hicho kama alivyonaswa na kamera yetu mjini Songea.
Mchuuzi wa vitunguu katika soko la kuu la Songea mkoani Ruvuma Bw Mkuya Omari, akipanga vitunguu hivyo chini huku maji machafu yanayotoka kwenye mabucha yaliyopo sokoni humo yakitiririka bila kuzingatia kanuni za afya,uuzaji wa vyakula wa aina hii ni hatari kwa walaji.
Muuza chumvi Ramadhan Said akisubiri wateja kando kando ya mtaa wa mkwepu mjini songea ambapo huuza kila kopo moja kwa shilingi 300,chumvi ya aina hii isiyokuwa na madini joto haifai kwa matumizi ya binadamu.
PICHA NA MUHIDIN AMRI WA GLOBU YA JAMII,RUVUMA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. hii chumvi ndo nzuri iliyowafanya wazee wetu waishi miaka mingi.wamekuja wajanja wanataka kuuza madini yao wamelazimisha tuwekewe kwenye chumvi hamna lolote zaidi ya kutupunguza nguvu za kiume tu na kutupunguzia umri.kula kitu natural hicho walichokuwa wanakula mababu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...