Mashabiki wa Yanga waliotinga katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuizomea Simba huku wakiwa na chupi Mkononi wametokanayo vichwa chini baada ya Simba ar es Salaa kuendeleza ubabe wake dhidi ya warabu baada ya kuichapa 2-0 timu ya Es Satif ya Algeria katika mchezo wa kuwanbia Kombe la Shirikisho barani Afrika. 

Magoli ya Simba yalifungwa kipindi cha pili na Mshambuliaji hatari Emmanuel Okwi kufuatia kazi nzuri ya Haruna Moshi Boban na goli la pili likifungwa nae Haruna Moshi Boban mwenyewe.
 
Mchezo wa marudiano unataraji kufanyika wiki mbili zijazo nchini Algeria ambapo Es  Setif italazimika kuifunga Simba 3-0 ili iweze kusonga mbele katika mashindano hayo. PICHA NA FATHER KIDEVU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Ushabiki una mipaka yake. Simba inaiwakilisha Tanzania, na sie kabla ya kuwa Simba au Yanga ni watanzania kwanza. Ni ukosefu wa hekima ndio unachangia baadhi ya watu kushabikia timu za nje. Watu wenye mchezo huu wanatakiwa waende hospitali kupima akili. Ona hawa hata wamebeba bendera ya Algeria!!! Tubadilike ndugu zangu. - Kilakshari

    ReplyDelete
  2. Well sasa kubeba chupi ndio nini?? hakuna njia nyingine ya kushabikia?? fool.
    Na kwanini CAF huwa wanapanga team zote wa waarabu zianzie ugenini?? hata kama nchi ina team mbili??
    Stupid CAF

    ReplyDelete
  3. Hivi hawa walioshika bendera ya Waalgeria wanawajua vizuri?! Hakuna watu wabaya na wanafiki kama hao, kwanza ni wabaguzi sana, pili ni wanaudini sana.Tuko nao hapa France ni wengi kwelikweli. Nakwamashabiki wa YANGA mkitaka kujua kuwa vichwa vyenyu ni maji yaliyochanganyika na tope la mto ruvu angalieni mpambano wa marudiano kama mtaona timu pinzania kwa ES SETIF kama itaishabikia simba, katu haitotokea.

    ReplyDelete
  4. Mtoto wa kabwela,SwedenMarch 26, 2012

    WaTanzania wamekuwa watu wa ovyo ovyo sana kwenye mambo mengi.Hamna uzalendo na Utaifa,yaani umekufa.Mimi inaniwia vigumu kuota Waalgeria wangeshabikia timu za nje na kubeba bendera ya nchi zingine,wakati timu zao zinavyocheza.Nchi nyingi uzalendo na Utaifa kwanza.

    Mtoto wa Kabwela,Sweden kusini

    ReplyDelete
  5. Nipo likizo Dar,nilikuwepo uwanjani..Mimi mpenzi wa Yanga lakini jana nikaenda kukaa jukwaa la Simba na kuwashangilia Simba.wale wapenzi wa Simba wenye nilipowaeleza kwamba mimi ni mpenzi wa Yanga lakini leo nashangilia Simba ya Tanzania..waliniona kama chizi fulani..Tuna Safari ndefu sana kwenye suala la Uzalendo..Niligundua kitu fulani vile vile humo uwanjani...Elimu nayo inachangia Uzalendo kukosekana?

    David V

    ReplyDelete
  6. Mimi ni shabiki mzuri wa Yanga ila siungi mkono asilani wanayanga wenzangu kushabikia timu za nje na kusahau utaifa wetu; hiyo inaonyesha ni jinsi gani tulivyo mambumbumbu na hatutakaa tafuulu kamwe kwa ajili ya kuendekeza ujinga wetu; sasa wewe ulienda na chupi nyekundu uwanjani ujui kuwa ni chupi anavyovaa mamako! haya na chupi yako bado umeshindwa vilevele.

    Algeria waarabu hao mwanawane hawana urafiki kamwe na ngozi nyeusi nakushangaeni mnavyojipeleka peleka huko na tubabaki kuwa kandambili daima yaani wa-kukanyagwa tu.

    Mdau wa Yanga

    ReplyDelete
  7. Mdau David V nakuunga Mkono,

    PANA UMUHIMU KUIRUDISHA JKT ILI KUAMSHA ARI NA MWAMKO WA UZALENDO AMBAO UMESHA ZAMA KABURINI.

    PANA MDAU ALIPINGA UWEPO WA JKT KTK MAONI YALIYOPITA KUWA HAINA UMUHIMU KUWEPO KWA VILE YEYE ALITUMIKIA MAFUNZO HAYO LAKINI HAKUONA FAIDA.

    WAKATI TUKIO KAMA HILI LINAASHIRIA KUANGUKA KWA UZALENDO MIONGONI MWETU SASA KWA KUWA VITU KAMA JKT LICHA YA DOSARI ZISEMWAZO HUJENGA UTAIFA NA UZELENDO ZAIDI.

    Ni aibu kubwa kwa Yanga kumshangilia Mwarabu...kwa Mtaji huo ipo kazi wenezetu nchi zingine Uzalendo kwanza hata kama wenyeji watacheza na 'Kivuli' lizima washangilie timu yao.

    Hivi kujitapa kwa Wana Jangwani kwa Unasaba wa kuwa wao ni Chama na Serikali kwa hapo ni sahihi kweli?

    ReplyDelete
  8. Uzalendo kwanza...huo ndio ushabiki wa hamnazo

    ReplyDelete
  9. Kwa kweli ndio maana Tanzania hatutajua mpira mpaka kufa kwetu, Yaani washabiki wa Yanga ndio wamekuwa wa algeria?! Hata wao wanatuona kuwa wajinga basi tu hatujui. MC KESSY

    ReplyDelete
  10. Kwa nini uende kushangilia simba.fikiria shabiki wa man city anaweza kuishgngilia man u.au wa barcelona aishangilie madrid amependa nini,atakuwa amelogwa apimwe wewe shabiki wa yanga au mamluki.ccm ifanye nini chadema haiwezi sifia huo ndo upinzani we vp?

    ReplyDelete
  11. David V umeongea - ELIMU ni bora kuliko mali.

    ReplyDelete
  12. kushangilia kwa chu.. huo ni utovu wa nidhamu hao watu ni malimbukeni kubeba nguo za ndani za dada zao au mwanamke yeyote anayemuheshimu hizo ni sifa za kijinga\\\\\\\\\\;;

    ReplyDelete
  13. Sasa ngojeni Mzunguko wa Pili huko kwao Algeria muone kama pana Mwarabu hata wa Timu pinzani ataishangilia Simba !

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...