Mgombea wa CCM jimbo la Arumeru Mashariki, Sioi Sumari akiumba kura kwa wananchi waliofurika kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika Maji ya Chai jimboni humo, jana. eneo hilo linadaiwa kuwa ndiyo ngome ya CHADEMA.
Mratibu wa kampeni za CCM, Mwigulu Nchemba akimnadi Sioi Sumari kwenye mkutano huo.
Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde 'akiwachana' CHADEMA kwenye mkutano uliofanyika Maji ya Chai ambako inasemekana ni ngome ya chama hicho.
Mwimbaji wa Kundi la Tanzania One Theatre (TOT) Khadija Kopa akihamasisha kwa wimbo wakati wa mkutano huo Maji ya Chai.
Wafuasi wa CCM wakishangilia wakati wa mkutano huo.
Sioi akifuaria umati wa wananchi waliohudhuria kwenye mkuatano huo.
Nambari wani heeee Nambari wani ni CCM
ReplyDeletewanaume tunapendeza ila mara nyingi tunaharibu katika soksi na mkanda.
ReplyDeleteMkewe inabidi awe mkali zaidi kuhakikisha mzee anatoka mchicha fulu hasa sasa ambapo anakuwa mbele ya kadamnasi mara kwa mara
Hao watoto vipi tena, mbona wengi hivyo?
ReplyDeleteMmmh kwa kweli wametikisa. Daah!!
ReplyDeleteIngekuwa mambo yetu yale ya 1947 hakuna vitu kama hivi tusingeweza kuona 'walivyotikisa'.!
Asante Mdau
na shida ya wanaume pale unapomwambia vua soksi shughuli huwa nzito utakuta either soksi imetoboka au harufu kali sana na hii ni 80%
ReplyDeletehawaruhusiwi kwani? ndo wapigakura wa kesho hao acha wasikilize sera zinazotekelezeka za chama makini cha Mapinduzi
ReplyDeleteSuala lisiwe kuwachana CHADEMA, chama tawala kinapaswa kuwaeleza wananchi kimetekelezaje sera zake na kina mikakati gani ya kurekebisha pale kilipokosea na kueleza mikakati yake mipywa ni ipi kwa kuihusisha na mbunge mpya wanaemnadi ili achaguliwe a wananchi. Kuwachana CHADEMA ambao hawako madarakani ni kupoteza lengo. Wanachi walio makini wanaweza kuwanyima kura.
ReplyDeleteKatika biashara ya Siasa ili muuze kwa Faida,,,msiangalie sana ukaribu na muhusika au undugu na huyo 'JOSHUA NASSARI' au mgombea la muhimu mnachotakiwa ni kuangalia Umakini wa muhusika na kuaminika kwake, sera na mwelekeo wake ili msije mkajutia uamuzi wenu hapo baadae!
ReplyDeleteLa kujitetea hapo ni kuhusu miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania ilivyopita hadi suala la umiliki wa ardhi likawa tete hapo Arumeru Mashariki.
ReplyDelete