Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye akikung'guta gitaa la solo leo  leo alipopata fursa ya kipekee kujiunga na Bendi ya Twanga Pepeta "Kisima Cha Buruduni" na kufanya nao mazoezi ndani ya ofisi za Aset. Baada ya kufanya makamuzi ya nguvu ilidhihirika wazi kwamba ukiachilia mbali siasa Nape ni msanii mkali wa kuimba, na kupiga vyombo mbalimbali vya muziki. Aidha Mkurugenzi wa Aset Asha Baraka alifurahishwa na kumshukuru sana Nape kuja kuwatembelea na kuwapa sapoti, vilevile alimuahidi kuwa nafasi yake itakua wazi kwenye bendi mara tu atakapo amua kuachia ngazi kutoka katika jukwaa la siasa na kuamua kujiunga katika tasnia ya muziki.
 Nape akipapasa Kinanda
Asha Baraka akimfurahia Nape wakati akifanya vitu vyake 
 Kija akimwangalia kwa makini Nape akipiga gitaa la Bass
Nape Nnauye akipiga Drums huku Msafiri Diouf akiimba

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Michuzi, huyu jamaa Diof alipotea hivi majuzi tu. Je alirudi lini na alikuwa wapi? Tupe habari.

    ReplyDelete
  2. Naamini kuwa mara nyingi watoto wengi hufata nyayo za baba au mama,huyu kijana wetu Nape kafuata nyayo za marehemu baba yake kwa wasiokuwa wakimfahamu marehemu Brg Nnauye alikuwa mwana siasa,na pia alipenda muziki sana kiasi kwamba alikuwa na chombo cha muziki nyumbani kwake.Hongera sana Nape,you are good boy.

    ReplyDelete
  3. Dah! Msafiri Diouf. Jamaa ana kipaji cha muziki lakini ndio hivyo tena. Kweli Mungu hakupi vyote.

    ReplyDelete
  4. papaa nape nadhani hii ndiyo inakufaa zaidi,siasani ni habari nzito kidogo.
    hapa unaweza kuwaburdiiiiisha watanzania kwa kina zaidi.sanasana ukizingatia pia lugha yako inavyofanana na hao,ushansoma mwana,kwani huko busara si lazima...
    chego

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...