Kaimu mkurugenzi wa halmshauri ya wilaya Namtumbo Constatino Mushi kushoto akimfariji mwanafunzi wa kidato cha 3 shule ya sekondari Runa wilayani humo Abdul Ngonyani aliyevunjika mkono wake wa kulia kufuatia gari walilokuwa wakisafiria kupinduka na kusababisha kifo cha mwanafunzi mmoja na wengine kujeruhiwa,katika ni baba mzazi Abdul Mang'inyuka,
Mwezeshaji wa mafunzo ya ukimwi kutoka idara ya maendeleo ya jamii ya halmshauri ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Pees Kamugisha akitoa mada wakati wa mdahalo wa wazi juu ya maambukizi mapya ya ukimwi kwa wanafunzi wa shule ya sekondari  st benedictine hanga, uliofanyika jana shuleni hapo,
Mwenyekiti wa kamati ya kudhibiti ukimwi ya halmshauri ya wilaya ya namtumbo ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa halmshauri hiyo Kassim Ntara akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya St Benedictine Hanga wakatri wa mdahalo wa siku moja juu ya kujikinga na maambikizi mapya ya ukimwi uliofanyika jana shuleni hapo,
Wanafunzi wa shule ya sekondari St Benedictine Hanga wilayani Namtumbo,wakiiangalia chini jana wakati wa mdahalo juu ya masuala ya ugonjwa wa ukimwi ulioendeshwa na idara ya maendeleo ya jamii ya halmshauri ya wilaya ya Namtumbo kupitia mpango wake wa elimu ya ukimwi mashuleni uliofanyika shuleni hapo,
Wanafunzi wa shule ya sekondari St Benedictine Hanga wilayani Namtumbo wakimsikiliza mwezeshaji wa masuala ya ukimwi kutoka idara ya maendeleo ya jamii ya wilaya hiyo Peres Kamugisha hayupo pichani wakati wa mdahalo wa siku moja juu ya namna ya kujiepusha na maambukizi mapya ya ukimwi uliofanyika shuleni hapo jana.PICHA NA MUHIDIN AMRI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Hii kali. Hawa wanafunzi mbona wana nidhamu ya uoga sasa wanaangalia chini kama kuku walio nyeshewa mvua jamani wakati watoto wenzao mijini umri wao wamechangamka na wanajua mambo mengi mwe mambo ya mikoani sijui..........kazi kwl kwl

    ReplyDelete
  2. Hizo ndio 'haya' za kike mdau, si nidhamu ya woga... Mtoto wa kike mwenye 'haya' anapendeza sana.. Sie mtoto mdogo anakukodolea macho kama mjusi kabanwa na mlango hadi unaogopa.

    ReplyDelete
  3. Kwa kweli walimu wana kazi ya ziada hapo watoto Confidence ZERO, Yaani hawajiamini kabisa! Kila mmoja anaogopa camera, duh! akiambiwa asimame aelezee jambo fulani ataweza kweli??

    ReplyDelete
  4. Mdau wa Tue Mar 20, 08:59:00 AM 2012, Hata mbuyu ulianza kama mchicha, hiyo pia ni process ya kuwajenga confidence maana kama watatembelewa mara mbili mara tatu na wageni basi watazoea wala si kwamba walimu wana kazi kubwa, confidnce inajengwa na uzoefu wa kujichanganya

    ReplyDelete
  5. HAWA waelimishaji naona walikuwa wanaongea mambo MAZITO SANA, watoto wa vijijini hawajui wanaogopa au anawaambia watumie kondomu wanaona ka anatukana, hayo mambo yaleteni Mjini maana hapo hata ukimwambia ajibu ataogopa kusema tttuuuuuuuuuuuu

    ReplyDelete
  6. aliekwambia wanaogopa kamera nani...kalagabaho wanaguswa n amambo wanayoelezwa..safi sana mtoa mada uliwagusa kunako...maana huwa hawaambiwi kbs mambo hayo na wazazi wao

    ReplyDelete
  7. Mdau ulitowa mada ya mwanzo hao watoto sio kama ni nidhamu tu bali inonekana tayari wengi wao tayari wana praktisi hayo mambo na hapo inaonesha kuna maneno yamewagusa kile wanachokifanya kama ishara ya kuhofia afya zao na maisha

    ReplyDelete
  8. Mi kwa mtazamo wangu somo kama hili at least angefundisha kijana mwenzao na sio baba/mjomba wao. Nadhani ingewasidia kuuliza maswali. Imagine unafundishwa reproduction au socialization na mama/baba yako.

    ReplyDelete
  9. WAACHENI WATOTO WADOGO WATOMBANE MBELE NA NYUMA HII FURAHA YA DUNIA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...