Mbunge mteule wa Arumeru Mashariki Mh. Joshua Nasari akiongea
baada ya kutangazwa  kuwa mshindi asubuhi hii huko Arumeru
Matokeo ya kura za Ubunge jimbo la Arumeru Mashariki yametangazwa sasa hivi na Msimamizi wa Uchaguzi na Mkurugenzi wa Wilaya ya Arumeru Bw Gracias Kagenzi amemtangaza mgombea wa CHADEMA Bw Joshua Nassari kuwa mshindi baada ya kupata kura 32,972 dhidi ya mpinzani wake wa karibu kutoka CCM Bw Sioi Sumari aliyepata kura 26,757

Matokeo kwa Vyama vingine sita vilivyoshiriki ni kama ifuatavyo
DP -77
NRA - 35
AFP - 139
UPDB - 18
TLP - 18
SAU - 22

Kwa mujibu wa Bw Kagenzi zaidi ya watu 120,000 walijiandikisha na aliojitokeza na kupiga kura walikuwa 60,696 ambapo kura halali zilikuwa 60,038 na zilizoharibika ni kura 661.

HUKO MWANZA NAKO...

Wakati huo huo, habari kutoka Mwanza zinasema CHADEMA kimeshinda  katika uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kirumba mkoani  Mwanza.

 Msimamizi wa uchaguzi huo, Bw. Aloyce Mkono, amemtangaza kuwa mshindi mgombea wa Chadema Mh Dany Kahungu kwa kura 2,938 dhidi ya  mgombea wa CCM  Mh Jackson Masamaki aaliyepata kura 2,131.

Wagombea wengine walioshindwa vibaya katika uchaguzi  ni pamoja na Mh Haji Issa wa CUF aliyepata kura 184, Mh Kasala Muhana wa UDP amepata kura 7 na Mh Athuman Jumanne wa NCCR Mageuzi aliyeambulia 0 katika uchaguzi huo .

Msimamizi huyo alisema kuwa uchaguzi huo umefanyika katika hali ya amani na utulivu,na kuwashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi huo na kuonyesha utulivu mkubwa wakati wa uchaguzi na zoezi la kutangazwa kwa matokeo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 65 mpaka sasa

  1. Sasa huyo wa NCCR aliyepata zero Ina maana hata yeye hakujipigia?

    ReplyDelete
  2. Tanzania is changing. Africa is changing!

    ReplyDelete
  3. What makes me wonder is where were the 60,000 voters who although registered did not turn up to vote?. I suspect majority of these absconders are students & youth in general. What a shame really. Now only 26% out of 100% have decided who would represent Arumeru East. Efforts should be made to educate young people on the importance of voting and driving changes in our society. alex bura, dar

    ReplyDelete
  4. SAFIIIIIII SANA JAMANI NIMEFURAHI MTOTO MBICHI MIAKA 26 TU ANAJIAMINI.CCM WAJIPANGE VIZURI 2015 WASIPANDE JUKWAANI NA KUTUKANA WAOMBE KURA TU KISTAARABU LUSINDE KAWAPONZA. WATAJIBEBA. LOWASA PRESHA INAPANDA PRESHA INASHUKA. POLENI SANA WANA CCM

    ReplyDelete
  5. Pipoooooooooooooz! Pawaaaaaaaaaaaaaa!
    Hongereni wananchi wa Arumeru. Mmeniwakilisha vyema kwa kweli! Duh!

    Na nyie wa upinzani nao it is high time mfanye kitu chenye akili. Kuna haja gani ya kushiriki uchaguzi hafu hata wewe mwenyewe hujipigii kura? Si nyote mngekubaliana mkawapoa Chadema? Ubinafsi tuuuuu! Aggrrrh!

    ReplyDelete
  6. huyo wa NCCR-Mageuzi , inaonyesha ALIKUWA MZUGAJI.

    ANATAKIWA AKAJIELEZE MAKAO MAKUU. HUYU NDIO WALE MAMLUKI WA CHAMA.

    NCCR-MAGEUZI OYEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE

    ReplyDelete
  7. Tumeshinda na Udiwani Mbeya na Songea!!Na bado...Tanzania childhood inakuja 2015!!

    David V

    ReplyDelete
  8. Ukisikia gharama chafu ya kuubeba Ufisadi matokeo yake ndio haya Arumeru Mashariki haya C.C.M,,,,,,,KAZI KWENU !

    ReplyDelete
  9. Awali zuri

    ReplyDelete
  10. MATOKEO YA UCHAGUZI ARUMERU MASHARIKI:

    Imethibitika kuwa,

    Zile zama za 'TAWALA ZA KIUKOO, na 'SIASA ZA KIUKOO' sasa zimekwisha !

    ReplyDelete
  11. ccm bye bye bye!!!!

    ReplyDelete
  12. Wapi CCM? Chezea Peoples Power ww. Big Congrats to Chedema. Very SOrry to CCM.

    ReplyDelete
  13. KUANGUKA KWA CHAMA TAWALA ARUMERU MASHARIKI:

    Kitu kibaya zaidi Mgombea wa Chama Tawala alikuwa 'Mgongoni mwa Fisadi' huku kada huyo wa Chama akiwa ni Baba Mkwe wake !

    ReplyDelete
  14. HONGERA SANA JOSHUA NA CHADEMA KWA UJUMLA, MNASTAHILI!!!!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  15. C.C.M ijifunze kuwa Siasa za Upendeleo hazifai kabisa tena mbaya zaidi kumkataa Sarakikya aliyekuwa safi akapewa mtu aliyekuwa na nasaba na Ukoo uliochafuka nchini !

    ReplyDelete
  16. Hata sioi na mshindi pia hawakujipigia kura, kwani walijiandikishia sehemu nyingine. Sioi hata huko Arumeru alikuwaga hajawahi kupafika, yeye alizowea mbezi beach. Karibu tena mbezi beach kaka, nimefungua mzigo mpya pale pale dukani kwangu, kuna suruali, mashati, pafyumu na hereni kibao, chaguo lako. Mama D.

    ReplyDelete
  17. hongereni wana ARUMERU kwa kupata uhuru.

    ReplyDelete
  18. Matokeo ya Uchaguzi wa Arumeru Mashariki,

    Mbona unaweka picha moja tu?

    Tunafahamu kuwa Michuzi wewe ni Kada wa Chama tawala na pia wewe ni Yanga Damu na Pia wewe ni Liverpool !

    ReplyDelete
  19. Fundisho na Aibu kubwa,

    CCM mnakubalika sana isipokuwa mnajishusha wenyewe kwa Siasa zenu za Upendeleo zitakazo wagharimu sana kwa kipindi hiki cha Dunia ya Mageuzi ya Kisiasa.

    Watu sasa sio ng'ombe wa kuelekezwa kila upande na wakaunga msafara.

    ReplyDelete
  20. SIOI ni muda wake sasa AOE kwa vile ameshapigwa mweleka !

    ReplyDelete
  21. Wala asiwe na wasiwasi wa kazi baada ya kushindwa Uchaguzi!

    Kazi ni kazi bora mkono wende kinywani, mwanaume hasa Mmasai hachagui kazi !

    Mgombea wa Chama Tawala aende akachunge ng'ombe wa baba mkwe wake Monduli.

    ReplyDelete
  22. Mkoa ule sio wenu ssm, mtu hadanganyiki pale sasa ivi. Poleni sana, hongera chadema!!!

    ReplyDelete
  23. Siyoi
    Lusinde
    Lowasa
    Mkapa
    Wassira
    Nape
    Mwigulu
    Wamekighalimu chama Arumeru hawa jamaa hawana mvuto kwa wapiga kura.
    Mwana CCM damu damu

    ReplyDelete
  24. Wala asiwe na wasiwasi wa kazi baada ya kushindwa Uchaguzi!

    Kazi ni kazi bora mkono wende kinywani, mwanaume hasa Mmasai hachagui kazi !

    Mgombea wa Chama Tawala aende akachunge ng'ombe wa baba mkwe wake Monduli.

    ReplyDelete
  25. Siasa ni biashara ngumu sana kwa sasa,,,ni sawa na kukalia kuti kavu!

    ReplyDelete
  26. Haya kumekucha TZ, wale waliosema kutumia helkopter ni hasara na kufilisika kwa CHADEMA mupo.

    ReplyDelete
  27. Bwana LIVINGSTONE LUSINDE aibuuuuu sijui utaificha wapi sura tako na mitusi yote ile uliyotukana! WELL DONE WANA ARUMERU.

    ReplyDelete
  28. Ahhh wapi Sioi aende SACCOS akachukue Mkopo aanze kuuza Vocha za simu Sokoni Tengeru !

    ReplyDelete
  29. Arumeru Oyeeeeeee!!!!


    Siasa za Manyau nyau sasa basi !

    ReplyDelete
  30. Hii ndo Demokrasia ya kweli, mapambano ndo yanaanza, Watanzania wa sasa hawaangalii sifa za chama wala ahadi hewa, amechoka na ufisadi, efedhuli na dhuluma. Binafsi sikuona mantiki ya Sioi kulazimishwa kugombea ilihali alikuwa hakubaliki. Na huo ndo ukweli. Si kila mtoto wa kigogo anaweza sisa jamani!

    ReplyDelete
  31. Kidumu Chama Cha CHADEMAAAAAAA!!!

    ReplyDelete
  32. CHADEMA OYEEEEEEE!!!!, nabado tunakuja taratibu, 2015, asiye na mwana abebe jiwe,asie na jicho aweke la mbuzi, Dr Slaa au Zitto Kabwe lazima wachukue nchia habari ndio hiyo. Mdau mbeba box Uk.

    ReplyDelete
  33. CHADEMA JUUUUUUUUUUUUUU!!! nlisema! nilisema! Vidume 5 vya CHADEMA vimewashinda viongozi wooooote wa CCM walioenda ARUMERU? hahaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!

    ReplyDelete
  34. CCM muache Siasa za Ki uongo uongo na kuubeba Ufisadi !

    Ama sivyo baadae mtafikia kuambulia Kura '0' kama huyo Mgombea wa NCCR Mageuzi !

    ReplyDelete
  35. Mtambo umezama barabara !

    tena bila ganzi wala kutemea mate,

    CHADEMA OYEEEEEEE !!!!!!!

    ReplyDelete
  36. Hongera Chadema! Michuzi na CCM yake Ziiiiiiiiiiii!

    ReplyDelete
  37. Big up wananchi wa Arumeru mashariki hamkuchagua chama mlichagua mtu atakayewawakilisha.
    Haiwezekani mtu anaishi mbezi beach dar es salaam aje tuu kutaka uongozi kisa kaoa kwa lowasa eti apewe uongozi, huo ni utovu wa nidhamu.
    Na hii serikali yetu ijifunze bila aibu viongozi mbalimbali wa chama walifunga safari eti kupiga kampeni, ZA NINI NA KWA LIPI MNAFIKIRI WATANZANIA HATUKO MACHO HUO UFISADI MNAOUFANYA JIONEENI AIBU TENA ABU KUMWA SANA KWA CHAMA TAWALA.

    michizi usinibanie hii comment yangu najua wewe ni c c m damu

    ReplyDelete
  38. Pepoles power mpo juuuuuuuuu!!! hii inaonyesha jinsi gani wananchi wameichoka CCM.nina uhakika 2015 CDM inaingia white house. Hongera sana CHADEMA tupo nyuma yako.

    ReplyDelete
  39. MWISHO WA MAFISADI TANZANIA UMEKARIBIA!

    ReplyDelete
  40. AJABU NA KWELI. Yaani hata yeye mwenyewe japo ukisema na mkewe anaweza kuwa amemsaliti mumewe ila ya kwake itakuwaje. Pongezi kwa aliyeshinda then sasa tufanye kazi tuache malumbano ya hapa na pale kwa kuwa mtu akishinda sio wa chama tena bali ni wa watu wote

    ReplyDelete
  41. UNCLE HABARI YA SAA HIZI?NAKUSALIMIA TUU.

    ReplyDelete
  42. Mabadiliko yanachukua mkondo wake taratibu.

    ReplyDelete
  43. hana mke? hata mke au sijui katibu au mwenyekiti wake wa eneo hilo? au ofisini yupo mwenyewe?
    funny

    ReplyDelete
  44. CCM tukusanye nguvu na ile mbinu yetu ya kuiba kura wataalam wako wapi? Mnajua tukikosa uongozi wa nchi chama kitakufa na ndo kinatuweka mjini?Cho nde chonde kama mbinu uwizi wa kura inagomba naomba tutafute mbinu mbadala. Degelavita.

    ReplyDelete
  45. Niliwaambia kwamba karibu tunafika pelekeni tu watoto shuleni hata kama hawapati kazi katika nchi yao wenyewe, faida yake ndo hii kwamba waelewa wazidi nasi tutafika salama katika mageuzi ya kisiasa na kiuchumi.amen.

    ReplyDelete
  46. Polisi wanapopiga watu mabomu bila kosa itazidisha kuigharimu CCM. Kile walichokifanya Mbeya ni kitendo cha kusikitisha sana

    ReplyDelete
  47. huyo wa Chadema Mbwembwe tu hana lolote

    ReplyDelete
  48. Labda hakuwa na sifa za kupiga kura. Usishangae ni kitu cha kawaida Bongo, hata mgombea wa CCM hajapiga.

    ReplyDelete
  49. wamegawanya ccm ilichukua jimbo la Igunga na wachadema wamechukua jimbo la Arumeru bado tena kivmbi cha 2015

    ReplyDelete
  50. Hongera sana sana kaka

    ReplyDelete
  51. Makomredi vipi hamkupeleka mgombea?

    ReplyDelete
  52. kwani huji wizi hata cheyo mwanza alisha wahi kuto kupata

    ReplyDelete
  53. People's Power Bana! we acha bana!
    Sauti ya watu ni sauti ya Mungu nimeamini!

    ReplyDelete
  54. Kwa kweli leo hii nimejisikia ni Mtanzania halisi, na ukweli ushindi wa Nassari unaipatia CCM heshima kubwa sana katika kukuza demokrasia.

    Nina hakika kuwa kama chaguzi zetu zote zitaendeshwa hivi na matokeo kutangazwa bila mizengwe ni dhahiri kuwa Tanzania itaendelea kuwa nchi ya amani na utulivu na mshikamano. Tuienzi hii hali kwa kutenda haki.

    Hongera Nassari chapa kazi sasa.

    ReplyDelete
  55. Ama kweli teja Chama Tawala habebeki!

    Pamoja na Libeneke kuwa upande wa wakubwa lakini haikusaidia kitu, chaliii wamepiga mwereka !

    ReplyDelete
  56. Hakika CCM sasa wamekwisha!

    This is good - it's indictive that our people are finally waking up.

    Siku zote nasema humu, waTanzania wa sasa siyo kama wa zamani zile za enzi za Nyerere na enzi za uhuru. Mtanzania wa sasa yuko 'aware'. Tumeamka na tumeshachoka 'kuburuzwa'!!

    Thank Goodness!!

    Buckinghamshire

    ReplyDelete
  57. Kampeni zingine na vigezo wala haviingii akilini.

    Ohhh Joshua Nassari hajaoa, hivi ni nani aliwaambia ya kuwa ktk Ndoa ndio kigezo cha uwezo wa Uongozi na Uadilifu?

    1.Ni wanagapi walio ktk Ndoa lakini bado ni wazinzi?

    2.Ni wangapi ktk Ndoa ambao ni wezi na si waadilifu?

    3.Je ni wangapi walio ktk ndoa na ndio kwanza wanazisaliti Ndoa zao?

    ReplyDelete
  58. Michuzi wewe ni Noma, umegoma kuweka comments kisa CCM imepigwa chini. Kweli globu ya jamii ina itikadi kali

    ReplyDelete
  59. Hongera sana Chadema. Ushauri kwa CCM: Muache utawala wa mabavu, kutetea ufisadi na ubinafsi. Mfuate maadili kama jina la chama chenu linavyoiitwa, Chama Cha mapinduzi kwa wananchi. Kauli mbiu ya maisha bora kwa kila Mtanzania iwe ya kweli kwa kila mtu na sio kwa wachache.

    ReplyDelete
  60. Pamoja na utu uzima wangu, leo hii nimetokwa na machozi, na wala sikumbuki mara ya mwisho nililia lini.

    Chadema, mbarikiwe sana. Tuna imani na ninyi.

    ReplyDelete
  61. Ahsante Mjomba Michuzi kweli Siasa unaiweza na umekomaa kama Kada wa CCM !

    Nimefurahi sana kuona maoni yangu yote ya 'Mabunduki' dhidi ya chama chako umeyaanika hewani !

    KUANGUKA KTK UCHAGUZI, NDIO ITASAIDIA MJIPANGE NA MJIREKEBISHE.

    HAIWEZEKANI ANKAL KILA UCHAGUZI UNASHINDA WEWE TU, KAMA VILE SISI WENGINE NA VYAMA VYETU NI MAITI !

    LAZIMA UKUBALI MATOKEO NA PIA UHUDHURIE MBUNGE AKIAPISHWA NA RAISI !

    HUO NDIO UKUBWA ANKAL NA UKOMAVU WA KISIASA !

    ReplyDelete
  62. Zama za SIASA za MABAVU na UJAMBAZI ZIMEKWISHAAAAA !

    UENEZI WA SIASA ZA KIUSANII UMEZIKWA KABURINI ARUMERU MASHARIKI JANA !

    ReplyDelete
  63. CHADEMA nyinyi ni watu wa mungu sna mana wte viongozi wenu ni wazuri sna kwa kuongea tu munajua

    ReplyDelete
  64. CHADEMA amka sasa;mbinu mpya ya PEOPLES'POWER imejibu.Ni kuanzia leo mrekebishe vitatizo ndani ya chama kabla havijaota mapembe. hapo sie waTZ wengi tutajiunga na Chama hiki chenye kutuonesha matumaini.

    ReplyDelete
  65. CCM mjipange upya,muache kuukumbatia ufisadi, muache siasa za kujuana za kupendelea watoto wa vigogo, siasa za uongo wa kujenga barabara wakati si kweli. Sioy hakuwa mmwanasiasa bali aliwekwa kwa kuwa ni mkwe wa fisadi na waliogopa kumuengua kwa vile fisadi angekuja juu. Wale walioachwa katika kura za maoni ndio wangefaa kuitete CCM.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...