Mshambuliaji wa timu ya Chelsea,Fernando Torres akishangilia goli lake kwa hisia kali sana aliloipachikia timu yake dhidi ya Timu ya Barcelona katika mchezo wa nusu fainali ya pili ya Kombe la UEFA.kwa mche zo huu wa leo uliomalizika kwa suluhu ya bao 2 - 2,na kuifanya timu ya Chelsea kutinga hatua ya fainali.
Wachezaji wa timu ya Chelsea wakishangilia goli zuri lililofungwa mBrazil,Ramires (pili kulia) wakati wa mchezo wao uliomalizika muda mfupi uliopita dhidi ya timu ya Barcelona.timu hizo zimefungana Bao 2 - 2,lakini kutokana na bao 1 waliloshinda Chelsea katika mchezo wa awali imefanya matokeo kuwa Barcelona 2 - 3 Chelsea na kuifanya timu hiyo kutinga fainali bila zengwe.
Pamoja na kwamba Chelsea walicheza pungufu baada ya Nahodha wao,John Terry kulambwa kadi nyekundu,lakini waliweza kuhimili mchezo huo mpaka mwisho.
jirani leo hataki kuongea na mtu maana shunguli yake ishaishaaaa.......kufungwa noma jamaniii...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. hakuna cha messi wala miss ni kipondo tuu hongereni wana wa darajani.
    mdau wa ukweli wa man uuuuuu

    ReplyDelete
  2. Pamoja na ushindi lakini tulibana zile ndude mwanzo mwisho mimi hadi sasa zinauma.

    ReplyDelete
  3. ndo mpira na wamekubali kushindwa na amani ilitawala. Terry kapata red card lakini refa hakupigwa ingekuwa Wanayanga???

    ReplyDelete
  4. ALL THE BEST CHELSEA.MMETUFURAHISHA AMAKWELI MAAJABU YA MWAKA KUCHEZA DAKIKA ZAID YA 70 PUNGUFU NA TIMU BORA DUNIANI,MMEPIGANA NI SHULE TOSHA KWA TIMU NYINGINE KUWA LOLOTE LAWEZEKANA

    ReplyDelete
  5. Zile gonga zilinifurahisha kuliko ushindi. Barca wanagonga ndinga jamani.

    ReplyDelete
  6. Mdau wa kwanza hapo juu:

    TOKA LINI mtu wa OLD TRAFFORD akampa shavu mtu wa STAMFORD BRIDGE?

    Watu wa Ligi ya Uingereza tatizo lenu mnao mtazamo kuwa Mpira ni UK tu !

    ReplyDelete
  7. kwa kweli wanastahili pongezi,kurudi 2-0 wakiwa pungufu sio kitu rahisi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...